Categories: Swahili Service

NI JAMBO LA ROHO

MFULULIZO: MAISHA NA NYAKATI ZA DAUDI

SOMO: 1 SAMWELI 16:1-13

 

Huu ni ujumbe wa kwanza katika mfululizo wa ujumbe huu juu ya maisha na nyakati zake Daudi. Hakuna maisha ya mtu anayelinganika na maisha ya Daudi.

  • Maisha ya Daudi ni maisha ya ukuu na pia maisha ya kawaida.
  • Daudi alikuwa mtu shujaa na pia mtu mwoga.
  • Daudi aliishi katika ushirika na Mungu na pia ushirika na mbinu za shetani.
  • Daudi alikuwa mtakatifu na pia mtu wa kawaida sana.
  • Mungu huwatumia watu wa kawaida kama wewe na mimi- 1 Wakorintho 1:26-31.

Hebu tujifunze:-

JINSI DAUDI ALIPOKEA UPAKO WAKE

Sauli- mtu aliyetupa mbao! – 1 Samweli 16:1-3.

  • Moyo wa Samweli ulivunjika kwa maana Mungu amemkataa Sauli kuwa mfalme Israeli.
  • Mfalme Sauli alikuwa chaguo la watu lakini chaguo lao halikumpendeza Mungu.
  • Mfalme Sauli alikuwa amemwasi Mungu mara tatu hivyo Mungu alimtema mfalme Sauli.
  1. 1 Sam.13- Sauli alimwasi Mungu kwa kutoa dhabihu wakati Samweli alichelewa kufika kwa ibada mle Gilgali- 1 Sam.13:5-14.
  2. 1 Sam. 14- Mfalme Sauli alitoa nadhiri ya haraka juu ya Jonathani- 1 Sam.14:24-31.
  3. 1 Sam.15- Mfalme Sauli alimwasi Mungu kwa kutomwangamiza mfalme Agagi.
  • Alipoulizwa juu ya kumwasi Mungu, mfalme Sauli alitoa vijisababu vingi- 1 Sam.15:24-25.
  • Sauli alikuwa mtu bila msimamo kamili, alikosa tabia.
  • Sauli alikuwa mtu wa hofu nyingi hivyo aliwapendeza watu kuliko Mungu!!
  • Sauli alifanya yaliyo mema machoni mwake, si mbele ya macho ya Mungu.
  • Sauli alikuwa mtu wa kuchanganyikiwa kuliko udhabiti wa tabia na mwelekeo.
  • Jinsi alivyo endelea kuishi hapa duniani, ndivyo alivyotenda maovu mbele ya Mungu.

Mungu alimtuma Samweli kwa nyumba ya Yesse.

  • Mungu alimwambia Samweli, kumwombolezea mfalme Sauli yatosha-  1; 16:1.
  • Mungu tayari alikuwa na mtu wake pembeni- 16:10.
  • Mungu anajali sana tabia kuliko heshima za wanadamu na maneno matupu.
  • Samweli alipendezwa sana na Eliabu lakini Mungu alitizama ndani mpaka roho ya mtu.
  • Pia Samweli alivutiwa na Abinadabu na Shama na ndugu zao. Lakini Mungu kumbe anatazama roho ya mtu na tabia kuliko sura na umbo- 16:7-10.

Daudi aliletwa kutoka malishoni.

  • Mungu anayatumia malisho ya kila aina kuwaandaa watu wake kwa kazi yake.
  • Mfalme kutoka kwa malisho.
  • Yusufu kutoka shimoni na gerezani.
  • Gideoni naye alikuwa amejificha katika pango.
  • Musa alikuwa jangwani.
  • Eliya alikuwa milimani ya Efraimu.
  • Elisha naye alikuwa shambani akilima.
  • Mungu kwanza anatujaribu na kazi ndogo ndogo kabla hajatupa kazi ya juu zaidi.
  • Mungu anatumia huduma ya chini kabla ya huduma ya juu zaidi kutengeneza mioyo yetu.
  • Daudi alichukuliwa bure na ndugu zake na pia baba yake- 1 Sam.16:11-13.
  • Daudi alikuwa ndiye wa heshima ya chini zaidi katika nyumba ya Yesse.
  • Lakini Mungu alikuwa anatazama roho na moyo wa Daudi.

JE, MOYO WA DAUDI ULIKUWA AJE?

  • Zaburi 15:1-3- Moyo wa kweli, ukamilifu, haki.
  • Zaburi 23:1-6- Moyo wa kumwamini Mungu- 14:1.
  • Zaburi 26:2- Moyo uliofunguliwa- Zaburi 139:23.
  • Zaburi 37:4-5- Moyo unaomtarajia Mungu na kumtegemea.
  • Zaburi 40:8- Moyo unaomkumbuka Mungu.
  • Zaburi 51:10, 17- Moyo unao tubu dhambi.
  • Zaburi 131:1- Moyo unao nyenyekea Mungu.

MOYO WA MWANADAMU KATIKA BIBLIA

  • Mungu anapomtafuta mtu, kwanza anapeleleza moyo wake. Haijalishi utaalamu, talanta, masomo, umbo, ujuzi na urembo la mtu.
  • Mioyo ni ya namna nyingi sana;-

Ovu- Mwanzo 6:5-6.

Kutoamini- Mwanzo 17:17.

Hofu- Mwanzo 42:28.

Ngumu- Kutoka 7:13-14, 22.

Hekima- Kutoka 28:3; 35:10, 1 Wafalme 3:12.

Kukata Roho- Hesabu 32:7.

Kuelewa- 1 Wafalme 3:12; 4:29.

KWA NINI MOYO WA MTU NI WA MAANA?

  • Kwa maana moyo ndio maskini na makao ya maisha yetu.
  • Mwanadamu anaishi katika moyo wake si katika nyumba yake.
  • Mioyo yetu ni uwanja wa mashindo ya Mungu na shetani.
  • Hivyo Mungu anatazama roho na moyo wa nyumbani, alipotazama moyo wa Daudi Mungu aliona:-
  1. Moyo wa ushujaa.
  2. Moyo wa ibada na sifa.
  3. Moyo wa kuuishwa (restorer).
  4. Moyo wa ufalme.
  5. Moyo wa kumpenda Mungu na neno lake- Zaburi 19.

 

MWISHO

  • Je, moyo wako ukoje?
  • Wengine wako na mwili na umbo lakini mioyo yao ni sumu.
  • Bwana nipe moyo safi.
root

Recent Posts

WHO IS SPEAKING TO YOU?

SERIES: DRAWING NEAR TO GOD TEXT: LAMENTATIONS 3:37 It reminds believers that God's word alone…

1 week ago

CHECHEA MSHINDI ALIYE NDANI YAKO.

MFULULIZO: MAISHA BILA VIZUIZI. SOMO: 1 YOHANA 5:4.   Wakristo wengi wanaishi maisha ya kushindwa…

1 week ago

THE GOD WHO BREAKS YOKES.

SERIES: THE GOD WHO NEVER FAILS. TEXT: ISAIAH 10:27.   God’s desire is that none…

2 weeks ago

THE REWARD OF SEEKING GOD

SERIES: DRAW NEAR TO GOD. TEXT: HEBREWS 11:6.   The Bible tells us that God…

3 weeks ago

JINSI YA KUTAMBUA NA KUVUNJA VIZUIZI VYA BINAFSI.

MFULULIZO: MAISHA BILA VIZUIZI. SOMO: WAAMUZI 6: 11-16   Moja ya vizuizi kubwa zaidi kwa…

3 weeks ago

GOD TURNS SHAME TO GLORY.

SERIES: THE HOD WHO NEVER FAILS. TEXT: ISAIAH 61:7   Shame is not the end…

4 weeks ago