MFULULIZO: AGANO LA UTAKASO.
SOMO: MWANZO 1:26-28.
Utawala na mamlaka ndiyo Agano la urithi wetu katika Yesu Kristo. Kupitia utakaso tumepewa nguvu na uwezo wa kutawala katika maisha, kutawala juu ya dhambi, utumwa, unyanyaso na nguvu zote za shetani. “Mungu akawabarikia, Mungu akawaambia zaeni, mkaongezeke, mkaijaze nchi na kuitiisha; mkatawale samaki wa baharini na ndege wa angani na kila kiumbe chenye uhai kiendacho juu ya nchi”-Mwanzo 1:28.
Utawala ndio mpango wa Mungu kwa mwanadamu tangu kuumbwa. Mungu aliumba mwanadamu kwa chapa na mfano wake.
Mungu hakumuumba mwanadamu aweze kunyanyaswa na hali yoyote au kuimbe chochote.
Mungu alimuumba mwanadamu kuwa mtawala, akampa mamlaka yote kudhibiti viumbe vingine vyote.
Mungu alimpa mwanadamu kumiliki, kutawala na kuwa na mamlaka juu ya kazi ya mikono yake.
Utawala na mamlaka hayo yote yalitolewa na Mungu kwa uhuru wake kuwa baraka juu ya mwanadamu.
Lakini, dhambi ilipoingia duniani yale mamlaka na utawala aliyopewa mwanadamu yaligeuka yakawa hofu, utumwa na kushindwa.
Lakini sasa katika Yesu Kristo, ukombozi wake umerejesha Wakristo kwa mahali pa kutawala na kuwa na mamlaka juu ya yote, iwe dhambi, unyanyaso na nguvu zote za giza na shetani.
Utakaso wa mamlaka na utawala Maanake ni kwamba mahali ambapo wengine wanatawalwa na dhambi, utumwa na nguvu za shetani, sisi tulio wana wa utakaso na ahadi za Mungu tunapata ushindi na tumepewa mamlaka na ushindi kutawala kila hali.
Utawala si jambo la kuvumilia katika vita vya maisha, lakini ni haki ya kutawala juu ya kila hali.
Utawala wetu si kukimbia hali ya kushindwa katika kila sehemu ya maisha.
Somo na ujumbe wetu leo ni wa maana sana wakati huu, kwa maana watu wengi wanaishi chini ya utumwa na kunyanyaswa na hali ya maisha ki-uchawi, vita vya kiroho, shida za jamii na uzito wa dunia hii.
Biblia inatuhakikishia kwamba walio wa Yesu Kristo ni zaidi ya washindi. Agano la utakaso linahakikishia wewe kwamba, hautakufa mahali wengine watakufa, hautaishia mahali wengine wataishia, hii ni kwa sababu Mungu amekutakasa, amekuweka wakfu, amekutenga upate kutawala.
Hebu tuone:-
MPANGO WA KWANZA WA MUNGU ULIKUWA NI KUTAWALA NA KUMILIKI.
Utawala na mamlaka ni mpango wa Mungu-Mwanzo 1:26.
Utawala ni baraka, si kung’ang’ania-Mwanzo 1:28.
Maanake utawala ni mamlaka na kumiliki-Zaburi 8:6.
Utawala unakutakasa kutokana na utumwa na unyanyaso-Luka 10:19.
DAMU YA YESU KRISTO NDIYO MSINGI WA UTAWALA NA MAMLAKA.
Damu ya Kristo inatupa ushindi juu ya adui-Ufunuo 12:11.
Damu ya Kristo inashinda mashtaka yote ya adui-Wakolosai 2:14.
Damu ya Yesu Kristo inakutakasa na hukumu na uaribifu wote-Kutoka 12:3.
Damu ya Yesu Kristo imetufanya Wafalme na makuhani-Ufunuo 5:10.
UTAWALA NA MAMLAKA JUU YA DHAMBI NA TAMAA ZA MWILI.
Dhambi haina nguvu juu yako-Warumi 6:14.
Roho Mtakatifu anatupa nguvu-Wagalatia 5:16.
Utawala na mamlaka zinahitaji nidhamu na utakatifu-1 Wakorintho 9:27.
Utawala unadumishwa kupitia utakaso-2 Timotheo 2:21.
MAMLAKA JUU YA NGUVU NA FALME ZA GIZA.
Yesu Kristo alizivua enzi na mamlaka-Wakolosai 2:15.
Utawala na mamlaka ni maisha ya ushindi katika vita vya kiroho-Waefeso 6:12.
Utawala na mamlaka yanapatikana kupitia maombi-Luka 18:1.
Utawala na mamlaka yanapatikana katika maombi-Mathayo 4:4.
MWISHO
TEXT: LUKE 2:1-14. The birth of Jesus Christ shattered spiritual, social and eternal barriers,…
TEXT: JOHN 3:16-17. Christmas unveils the divine mission behind the birth of Jesus Christ;…
MFULULIZO: KRISMASI NI KUFUNULIWA KWA YESU KRISTO. SOMO: LUKA 2:8-14. Krismasi inafunua jibu la…
SERIES: CHRISTMAS IS CHRIST. TEXT: JOHN 1:1-14. Christmas is the divine moment when God…
TEXT: ISAIAH 53:1-12. The son of man came to seek and save that which…
SERIES: CHRISTMAS IS JESUS CHRIST. TEXT: MATTHEW 1:21 Jesus Christ is the savior of…