LUKA 2:36-38
Ana ni moja wao aliyechangia pakubwa kuzaliwa kwa Yesu Kristo. Leo tutazame maisha ya Nabii Ana. Ana kwa siku moja aliyatimiza mapenzi ya Mungu pamoja na kutimiza hatima ya maisha yake. Ana alipata mikosi katika maisha Yake, lakini kwa Imani Ana aliyashinda yote. Ana ni kielelezo chema cha jinsi ya kuishi kwa Imani. Ana hau Hanna maana yake jina ni Neema hau mweye kuneemesha. Babaye Ana alikuwa Fanueli wa kabila la Asheri. Fanueli ni jina ambalo Yakobo alipaita mahali alipo shindana mweleka na Mungu (Mwanzo 32:24). Maana yake Fanueli ni “uso wa Mungu”. Asheri maana yake ni “furaha”. Asheri alikuwa mwana wa nane wa Yakobo kwa wana 12 (Mwanzo 30:13)
Yakobo alipowabarikia wanawe kabla ya kufa kwake, alimsema Asheri “Asheri chakula chake kitakuwa kinono naye atatoa tunu za kifalme” (Mwanzo 49:20) naye Musa alimsema Asheri “Asheri abarikiwe kwa watoto, na akubaliwe katika nduguze, na achovye mguu wake katika mafuta.” (Kumbu kumbu 33:24). Asheri walikuwa kabila la kubarikiwa na mali na kuzaa watoto wa kifalme. Yoshua naye aliwapatia Asheri inchi nzuri sana kuwa urithi na miiki yao, karibu na bahari ya kati. Wanawake wa Asheri walikuwa warembo zaidi hivyo wakaolewa na wafalme! (Yoshua 19:24-31). Lakini kwa Baraka hizi zote Asheri aliishi katika majaribu mengi sana – waliendelea kuishi pamoja na wakanaani (Waamuzi 1:31-40) muamuzi Debora aliwanena Asheri (Waamuzi 5:17). Asheri alikuwa na imani Dhaifu, mambo ya kiroho hayakumpendeza Asheri. Hakupenda vita vya kiroho. Baadaye Asheri walichukuliwa mateka katika uamisho, hata ingawa hivyo pale Yerusalemu palikuwa na Ana—nabii mke, binti yake Fanueli mtu wa Asheri!! Neema yake Mungu inaenda upande upande kwa mataifa yote. Hebu tutazame:-
I. ANA ALIYABANDILISHA MAOVU KUWA MEMA (TURNING NAGATIVES INTO POSITIVES) KWA IMANI.
II. ANA ALIJIFICHA HEKALUNI (ZABURI 68:5, 146:9
III. ANA ALITANGAZA UWEPO WA BWANA HEKALUNI.
MWISHO
MFULULIZO: AGANO LA UTAKASO. SOMO: KUTOKA 12:12-13. Damu ya Yesu Kristo ndiyo mhuri wa…
SERIES: SUPERNATURAL ADVANCEMENT. TEXT: HABAKKUK 3:19. The journey of fulfilling your destiny does not…
SERIES: THROUGH THE BOOK OF COLOSSIANS. TEXT: COLOSSIANS 3:15 Thankfulness is a great attitude…
SERIES: THE ANOINTING. TEXT: EZEKIEL 47:1-5 There are levels of the anointing and each…
MFULULIZO: AGANO LA UTAKASO. SOMO: ESTA 2:15-18. Kibali cha Mungu ndicho kinacho watenga watoto…
SERIES: THE GOD WHO NEVER FAILS. TEXT: HAGGAI 2:6-9. God has the power to…
View Comments
Ana nabii mke aliamua kukaa hekaluni na kuomba bila kukoma juu ya Bwana. Kwa maana hiyo alikuwa anatayarisha mazingira bora kabisa ya ujio wa Kristo na maisha yake ndani ya kukataliwa.
Jina la Bwana libarikiwe. Asante kwa neno hili
Najifunza kuzingojea ahadi ya Mungu Kwa kuomba bila kukata tamaa kama Nabii Ana