ANA – NABII MKE

LUKA 2:36-38

Ana ni moja wao aliyechangia pakubwa        kuzaliwa kwa Yesu Kristo. Leo tutazame     maisha ya Nabii Ana. Ana kwa siku moja     aliyatimiza mapenzi ya Mungu pamoja na kutimiza hatima ya maisha yake. Ana alipata mikosi katika maisha Yake, lakini kwa Imani Ana aliyashinda yote. Ana ni kielelezo chema cha jinsi ya kuishi kwa Imani. Ana hau Hanna maana yake jina ni Neema hau mweye kuneemesha. Babaye Ana alikuwa Fanueli wa kabila la Asheri. Fanueli ni jina ambalo Yakobo alipaita mahali alipo shindana mweleka na Mungu (Mwanzo 32:24). Maana yake Fanueli ni “uso wa Mungu”. Asheri maana yake ni “furaha”. Asheri alikuwa mwana wa nane wa Yakobo kwa wana 12 (Mwanzo 30:13)

Yakobo alipowabarikia wanawe kabla ya kufa kwake, alimsema Asheri “Asheri chakula chake kitakuwa kinono naye atatoa tunu za kifalme” (Mwanzo 49:20) naye Musa alimsema Asheri “Asheri abarikiwe kwa       watoto, na akubaliwe katika nduguze, na achovye mguu wake katika mafuta.” (Kumbu kumbu 33:24). Asheri walikuwa kabila la kubarikiwa na mali na kuzaa watoto wa         kifalme. Yoshua naye aliwapatia Asheri inchi nzuri sana kuwa urithi na miiki yao, karibu na bahari ya kati. Wanawake wa Asheri walikuwa warembo zaidi hivyo wakaolewa na wafalme! (Yoshua 19:24-31). Lakini kwa Baraka hizi zote Asheri aliishi katika majaribu mengi sana – waliendelea kuishi pamoja na wakanaani (Waamuzi 1:31-40) muamuzi Debora aliwanena Asheri (Waamuzi 5:17). Asheri alikuwa na  imani Dhaifu, mambo ya kiroho hayakumpendeza Asheri. Hakupenda vita vya kiroho. Baadaye Asheri walichukuliwa mateka katika uamisho, hata ingawa hivyo pale    Yerusalemu palikuwa na Ana—nabii mke, binti yake Fanueli mtu wa Asheri!! Neema yake Mungu inaenda upande upande kwa mataifa yote. Hebu tutazame:-

 

I.  ANA ALIYABANDILISHA MAOVU KUWA MEMA (TURNING NAGATIVES INTO POSITIVES) KWA IMANI.

  • Kuwapo kwa Ana Hekaluni mle Yerusalemu kwa onyesha maajabu ya uaminifu wa Mungu.
  • Ana alikuwa mabaki ya kabila lake, mwenye Imani wakati kabila lake Asheri walimwacha Mungu wao.
  • Ana kama Simeoni aliishi kwa kutarajia na kungojea wokovu wa Bwana.
  • Imani ya Ana inaonekana katika machache yaliyoandikwa na Luka.
  • Ana alikuwa mjane wa miaka 84. aliolewa akiwa miaka 14, na akaishi na mme wake miaka 7 hivyo Ana alikuwa na miaka 105. aliachwa na mme wake akiwa na umri wa miaka 21.
  • Ana angeolewa tena lakini aliamua kumuishia Mungu na kumtumikia katika maombi na kufunga saumu.
  • Biblia inasema ANA “haondoki katika hekalu, ila huabudu usiku na mchana kwa kufunga na kuomba.
  • Wakati wa biblia mme alikuwa ni bima ya mwanamke hivyo kufiwa na mume kuliacha mjane katika mikono ya wezi (social parasites or parasites of society)
  • Pamoja na sheria ya Musa, waisraeli waliwanyanyasa wajane sana, kama Kenya ya leo (Ayubu 22:8-11, 24:2,21)
  • Ana alijiolesha kwa Mungu (I Wakorintho 7:29-35).

 

II.  ANA ALIJIFICHA HEKALUNI (ZABURI 68:5, 146:9

  • Ana alijua Mungu na kao lake takatifu. Ana alipofiwa na mme wake mlinzi wake, Ana alimkimbilia mme wa kweli yaani Yehova.       Ana alikaa katika nyumba ya Bwana wake, haondoki.
  • Usiku na mchana, siku baada ya siku, kwa miaka 84. Ana aliomba na kufunga kwa ajili ya watu wake Asheri.

 

III.  ANA ALITANGAZA UWEPO WA BWANA HEKALUNI.

  • Ana alimshukuru Mungu na wote waliokuwa wakiutarajia ukombozi katika Yerusalemu.
  • Ana aliwatolea wengine habari zake Mkombozi Kristo.
  • Haijalishi mda ulipongojea ahadi za Mungu kwako, haijalishi jinsi hali yako ilivyo mbele ya macho ya watu wengine, mtafute Bwana, jifiche katika uwepo wake, watangazie wengine habari zake.                                             Siku moja tu, Ana alimwona Mwokozi wake.

 

MWISHO

  • Ana alikuwa mke Nabii, hakupoteza Imani yake juu ya miaka mingi, Ana hakupatwa na machungu ya moyo hata kwa kufiwa na mme wake. Ana alikuwa mwombezi 24/7. Ana alimtambua Kristo, akashukuru.         Ana alitangaza habari hizi kwa wote walio mwamini Mungu.
  • Katika hali yote endelea kutembea na Bwana mpaka mwisho.

 

The following two tabs change content below.
Rev, Dr. Willy Mutiso is the Senior Pastor at First Baptist Athiriver. He is widely known for his practical and dynamic teaching style which helps people apply the timeless truths of Scripture to their everyday lives.

Latest posts by Rev, DR. Willy Mutiso (see all)

Rev, DR. Willy Mutiso

Rev, Dr. Willy Mutiso is the Senior Pastor at First Baptist Athiriver. He is widely known for his practical and dynamic teaching style which helps people apply the timeless truths of Scripture to their everyday lives.

View Comments

  • Ana nabii mke aliamua kukaa hekaluni na kuomba bila kukoma juu ya Bwana. Kwa maana hiyo alikuwa anatayarisha mazingira bora kabisa ya ujio wa Kristo na maisha yake ndani ya kukataliwa.
    Jina la Bwana libarikiwe. Asante kwa neno hili

Share
Published by
Rev, DR. Willy Mutiso

Recent Posts

DAMU YA UTAKASO.

MFULULIZO: AGANO LA UTAKASO. SOMO: KUTOKA 12:12-13.   Damu ya Yesu Kristo ndiyo mhuri wa…

1 day ago

KEY TO DIVINE SPEED.

SERIES: SUPERNATURAL ADVANCEMENT. TEXT: HABAKKUK 3:19.   The journey of fulfilling your destiny does not…

1 day ago

BE YE THANKFUL TO GOD.

SERIES: THROUGH THE BOOK OF COLOSSIANS. TEXT: COLOSSIANS 3:15   Thankfulness is a great attitude…

1 day ago

LEVELS OF THE ANOINTING.

SERIES: THE ANOINTING. TEXT: EZEKIEL 47:1-5   There are levels of the anointing and each…

5 days ago

UMETAKASWA KUPOKEA KIBALI.

MFULULIZO: AGANO LA UTAKASO. SOMO: ESTA 2:15-18.   Kibali cha Mungu ndicho kinacho watenga watoto…

1 week ago

THE GOD WHO SHIFTS THE HEAVENS IN YOUR FAVOR.

SERIES: THE GOD WHO NEVER FAILS. TEXT: HAGGAI 2:6-9.   God has the power to…

1 week ago