Categories: Swahili Service

CHIMBUA VISIMA YA MAOMBI

MFULULIZO: KUPENYA KUSIO KWA KAWAIDA

SOMO MWANZO 26:18; MARKO 16:15-20

 

Ikiwa tutapata kuwa na nguvu, ishara maajabu, uponyaji na miujiza kama kanisa la kwanza katika kitabu cha Matendo ya Mitume, ni lazima kuweka maombi katika mstari wa kwanza kama wao.

“Isaka akarudi akavichimbua vile visima vya maji walivyovichimba siku za Ibrahimu babaye; maana wale Wafilisti waliokuwa wamevifukia baada ya kufa kwake Ibrahimu, Naye akayaita majina kufuata majina alivyoviita baadaye”-Mwanzo 26:18.

Leo hii tunataka kuchimba upya visima walivyochimba kanisa ya kwanza!!

“Utukufu wa mwisho wa nyumba hii utakuwa mkuu kuliko utukufu wake wa kwanza, akasema Bwana Wa Majeshi, na katika mahali hapa Nitawapa amani asema Bwana  Wa Majeshi-(Hagai 2:9).

Hekalu la sasa halijawahi kuwa kuu kuliko lile la matendo ya mitume!!

Ni lazima sasa nasi tupigane sana kiasi tupate kupenya zaidi kuliko kanisa la Agano Jipya.

Tutapata Nguvu zaidi ya kanisa la kwanza ikiwa tutapata kuwa na njaa na kiu ya makuu ya Mungu, kwa kukataa maisha ya kawaida!!

Yesu Kristo alisema “Akafundisha Yesu Kristo akasema , Je haikuandikwa , Nyumba yangu itaitwa Nyumba ya sala kwa mataifa yote-(Marko 11:17).

Ikiwa tunataka kuona Nguvu zaidi, ishara zaidi, maajabu zaidi, uponyaji zaidi, na miujiza zaidi kama jinsi kanisa la Agano Jipya, katika Matendo ya mitume ni lazima kuweka maombi mbele kama walivyofanya wale.

Yesu Kristo anataka Nyumba hii, iweze kuwa nyumba ya maombi, kwa mataifa yote.

Lakini Je, Hii Nyumba inaweza kuwa nyumba ya maombi kwa mataifa yote Njia gani?

Hebu tutazame:-

MSINGI WA MAOMBI KATIKA KITABU CHA MATENDO: (Matendo 1:14-24, 2:1-4; 2:42).

  • Tunapotazama sana, tunaona mambo tatu:-

Uwepo wa Mungu:

  • Wakristo wa kwanza walitarajia sana kuhisi uwepo wa Yesu Kristo, kupitia kwa Roho Mtakatifu katika kila Ibada na mikutano yao kila walipokutanika!!
  • Kulikuwa wakati Wakristo wakaja kanisani kukutana na Mungu.
  • Lakini Leo Wakristo wakuja kanisani kuimba Nyimbo juu ya Mungu.

Nguvu za Mungu: 

  • Kanisa la kwanza walitarajia kuona Nguvu zisizo za kawaida, Nguvu za Mungu Katikati ya mikutano na maombi yao-(Marko 16:15-20).

Katika kanisa la Agano jipya, kanisa la kwanza, kila mtu alishiriki ibada na kazi ya Mungu!!

  • Katika kanisa la kwanza kila mshiriki alihusika, walitarajia kutumika, kulingana na muongozo wa Roho Mtakatifu.
  • Kila mshiriki alijua karama yake ya kiroho na kushiriki vilivyo katika karama zao.

JE, TUNASOMA NA KUJIFUNZA KITU GANI KATIKA MATENDO 3:1-11)?

Kwanza, maombi ndiyo maana zaidi. 

  • Petro na Yohana walienda hekaluni kwa “lisaa la maombi”
  • “Nyumba yangu itaitwa Nyumba ya maombi”
  • Wala si nyumba ya sifa, mahubiri, nyimbo, michezo, chakula. Hata Ingawa mambo haya yote ni ya maana sana, lakini ni “Nyumba ya Maombi kwa mataifa yote.”

Tunahitaji kuzidisha matarajio yetu kwamba Mungu atende kitu, ajidhiirishe mbele yetu kila kunapokutwa katika Nyumba yake na katika kila ushirika wa watu wake.

  • Petro na Yohana waliponena na yule mtu kiwete katika mlango wa hekalu, yule kiwete alitarajia kitu kutoka kwao.

Ni lazima tupokee Nguvu za Mungu kwanza kabla hatujawapa watu hizo Nguvu.

  • Petro alimwambia yule kiwete “fedha na dhahabu sina lakimi nilicho nacho nakupa wewe ….. katika jina la Yesu simama na uende.”
  • Petro alijua alibarikiwa hili awe baraka-Tumepokea bure– Bure tuwape watu.
  • Petro na Yohana walikuwa Jasiri-(Matendo 4:13).

HEBU TAZAMA MAOMBI YAO-(Matendo 4:23-24; 29-31).

Kwanza tunahitaji kuomba Pamoja kama kanisa.

Waliyainua macho yao, sauti zao kwa Mungu kwa Pamoja.

  1. Tukumbuke Mungu ni nani – Muumba-
  2. Tuombe Mungu kufanaya ishara, maajabu, miujiza. Maajabu yanafanya watu kuona ajabu!!
  3. Tunahitaji kujazwa Roho Mtakatifu upya kila (Matendo 10:38)

MWISHO.

  • Bwana anataka sisi sote kurudia upendo wetu wa kwanza, kwake.
  • Mungu anafanya kazi na walio na matarajio kwanza.
  • “Nyumba yangu itaitwa nyumba ya maombi kwa mataifa yote.
  • Je, unatarajia Nini leo kutoka kwa Mungu? Hebu tuombe!!
The following two tabs change content below.
Rev, Dr. Willy Mutiso is the Senior Pastor at First Baptist Athiriver. He is widely known for his practical and dynamic teaching style which helps people apply the timeless truths of Scripture to their everyday lives.

Latest posts by Rev, DR. Willy Mutiso (see all)

Rev, DR. Willy Mutiso

Rev, Dr. Willy Mutiso is the Senior Pastor at First Baptist Athiriver. He is widely known for his practical and dynamic teaching style which helps people apply the timeless truths of Scripture to their everyday lives.

Recent Posts

MSAADA WA MUNGU WAKATI WA MATESO.

MFULULIZO: MAISHA BILA VIZUIZI. SOMO: ZABURI 46:1.   Biblia inatuakikishia kwamba Mungu wetu ni “Msaada…

3 weeks ago

GOD GUIDES OUR DESTINIES.

SERIES: THE GOD WHO NEVER FAILS. TEXT: PROVERBS 3:5-6.   Every destiny is a divine…

3 weeks ago

PUT OFF AND PUT ON

SERIES: THROUGH THE BOOK OF COLOSSIANS. TEXT: Colossians 3:5-10   We have put off the…

3 weeks ago

GOD OF THE BREAKTHROUGHS

SERIES: THE GOD WE SERVE TEXT: 2nd SAMUEL 5:17-20   Breakthroughs are divine interventions that…

4 weeks ago

WHO IS SPEAKING TO YOU?

SERIES: DRAWING NEAR TO GOD TEXT: LAMENTATIONS 3:37 It reminds believers that God's word alone…

1 month ago

CHECHEA MSHINDI ALIYE NDANI YAKO.

MFULULIZO: MAISHA BILA VIZUIZI. SOMO: 1 YOHANA 5:4.   Wakristo wengi wanaishi maisha ya kushindwa…

1 month ago