MFULULIZO: YAKOBO; ALIFANYA MIEREKA NA MUNGU.
SOMO: MWANZO 30-31
Tunaishi katika ulimwengu ambao watu wanatafuta sana kwa bidii fedha, utajiri, mali na ustawi. Kustawi ndio lengo la wengi wetu. Naye Mungu pia anapenda kutupa ustawi maana ni ahadi yake kustawi kwetu. Mungu alimwahidia Yakobo kumbariki na kumpa ustawi, hivyo Yakobo alistawi sana katika miaka ya maisha ngumu sana mle Harani. Mwanzo 30:43- “Kuwa hiyo mtu huyo akazidi mno, akawa na wanyama wengi na vijakazi, watumwa, ngamia na punda.” Katika kuishi kwake Yakobo, katika nyumba ya Labani mjomba wake na pia shemeji, Yakobo alipokea udanganyifu kwa udanganyifu. Yakobo alidanganywa sana na Labani, pia katika nyumba yake Yakobo palikuwa na vita vikali katika wake zake Lea na Raeli. Labani pia alimdanganya Yakobo kimshahara wake. Yakobo kweli alikimbia Beer-Sheba kutorokea uhasama lakini akapata zaidi mle Harani. Hivi ndivyo Yakobo anawaambia wake zake. Mwanzo 31:6-7-“Ninyi mmejua ya kwamba kuwa nguvu zangu zote nimemtwikia baba yenu. Na baba yenu amenidanganya akabadili mshahara wangu mara kumi, lakini Mungu hakumwacha kunidhuru.” Labani alipoona Yakobo anastawi, Labani alibadili nia na sheria za kazi. Labani alijaribu sana kumweka Yakobo chini. Kwa sababu ya shida, Yakobo aliamua kurudi Beer-Sheba kwa baba yake Isaka. Mwanzo 30:25- “Ikawa Raeli alipomzaa Yusufu, Yakobo akamwambia Labani, nipe ruhusa niende kwetu na kwenye nchi yangu.” Labani alijitoa kumsaidia Yakobo-Mwanzo 30:31- “Akamuuliza, nikupe nini? Yakobo akasema, usinipe kitu, ukinifanyia neno hili, nitalisha wanyama wako tena na kuwalinda.” Yakobo hakutaka kuwa mdeni kwa yeyote yule. Yakobo alikubali kuwalisha kondoo wa Labani, walio wa madoadoa na marakaraka na pia mbuzi walio madoadoa na marakaraka kama mshahara wake. Mungu akiamua kukubariki hakuna atakayekataa. Yakobo alijiweka katika mkono wa Mungu wake, kamtumaini Mungu kwa matokeo ya kazi ya mikono yake- Mwanzo 30:33-36. Mwishowe Yakobo aliamua kurudi nchi ya babaye- Mwanzo 31:3; 17-18. Kwa miaka 20 miaka ya shida Yakobo alipata kuwa tajiri sana akastawi zaidi na zaidi- Mwanzo 30:43; Mwanzo 32:10. Tunakuwa zaidi katika shida zetu kuliko wakati wa utulivu na amani.
KANUNI ZA USTAWI: BARAKA ZINAFUATA UTII
KANUNI ZA USTAWI: UWE NA TAMAA YA KUFAULU NA KUSTAWI- Mwanzo 30:30
KANUNI ZA USTAWI: BIDII YA KAZI INALIPA
KANUNI ZA USTAWI: UWE MKWELI
KANUNI ZA USTAWI: USITOROKE UTOSHELEVU WA MUNGU
KANUNI ZA USTAWI: TAFUTA AMANI NA WATU WOTE
KANUNI ZA USTAWI: FANYA UHUSIANO WAKO NA MUNGU KUWA MKUU
MWISHO
MFULULIZO: AGANO LA UTAKASO. SOMO: KUTOKA 12:12-13. Damu ya Yesu Kristo ndiyo mhuri wa…
SERIES: SUPERNATURAL ADVANCEMENT. TEXT: HABAKKUK 3:19. The journey of fulfilling your destiny does not…
SERIES: THROUGH THE BOOK OF COLOSSIANS. TEXT: COLOSSIANS 3:15 Thankfulness is a great attitude…
SERIES: THE ANOINTING. TEXT: EZEKIEL 47:1-5 There are levels of the anointing and each…
MFULULIZO: AGANO LA UTAKASO. SOMO: ESTA 2:15-18. Kibali cha Mungu ndicho kinacho watenga watoto…
SERIES: THE GOD WHO NEVER FAILS. TEXT: HAGGAI 2:6-9. God has the power to…