MFULULIZO: KRISMASI NI KUFUNULIWA KWA YESU KRISTO.
SOMO: LUKA 2:8-14.
Krismasi inafunua jibu la Mungu la furaha katika dunia ya dhiki, shida na farakano.
“Malaika akawaambia, msiogope; kwa kuwa mimi ninawaletea habari njema ya furaha kuu itakayokuwa kwa watu wote”-Luka 2:10.
Dunia hii tunayoishi ni mahali pa dhiki, shida, magumu ya uchumi, magonjwa, hofu na kuchanganyikiwa kiroho.
Mioyo mingi imevunjika na imebeba mizigo mizito sana-Mathayo 11:28-30.
Furaha katika maisha, jamii, dunia na nchi imekuwa jambo la mbali sana. Hakuna furaha duniani.
Katika dunia ya shida, Mungu alileta Krismasi kama njia yake kuleta furaha katika ulimwengu.
Kuzaliwa kwa YESU KRISTO hakukufanyika katika ikulu ya furaha na amani, lakini kulifanyika wakati wa ukoloni na utumwa wa Roma duniani kote.
Mungu hangojei kuwa na amani hili aweze kuachilia furaha yake.
Krismasi inatuonyesha kwamba furaha sio ukosefu wa dhiki na shida, lakini ni kuwepo kwa YESU KRISTO.
Krismasi hivyo, si tu sherehe ya siku fulani, lakini ni tangazo ya kwamba mbingu imeleta furaha kwa ulimwengu wa dhiki.
Furaha hii sio ya wakati au msimu, bali ni furaha ya milele, furaha ya nguvu, furaha inaobadilisha maisha. Hebu tutazame:-
KRISMASI NI TANGAZO YA FURAHA YA MUNGU KWA ULIMWENGU WA HOFU.
Furaha inapigana na hofu-Luka 2:9-10.
Furaha ni ujumbe wa mbinguni-Luka 2:10.
Furaha ya mbinguni ni kwa watu wote-Luka 2:10.
Furaha ya Mungu huvunja roho ya kudhoofika na kuvunjika moyo-Isaya 61:3.
KRISMASI ULETA FURAHA KATIKA DHIKI.
Dhiki ni lazima hapa duniani-Yohana 16:33.
Furaha imo ndani ya Kristo, si katika hali ya dunia na maisha-Yohana 15:11.
Furaha ya Mungu inaleta amani panapo taharuki-Wafilipi 4:7.
Furaha ya Mungu inatupatia nguvu kama Wakristo-Nehemia 8:10.
KRISMASI UREJESHA FURAHA KATIKA MIOYO ILIYOVUNJIKA.
Mungu uponya mioyo iliyovunjika-Zaburi 147:3.
Furaha inatoka kwa Roho Mtakatifu.
KRISMASI INAFUNGULIA FURAHA YA MILELE KWA ULIMWENGU.
Yesu Kristo ndiye mfalme wa amani na furaha-Isaya 9:3.
Furaha yetu itakamilika katika utukufu wa Mungu mbinguni-Ufunuo 21:4.
MWISHO
TEXT: LUKE 2:1-14. The birth of Jesus Christ shattered spiritual, social and eternal barriers,…
TEXT: JOHN 3:16-17. Christmas unveils the divine mission behind the birth of Jesus Christ;…
SERIES: CHRISTMAS IS CHRIST. TEXT: JOHN 1:1-14. Christmas is the divine moment when God…
TEXT: ISAIAH 53:1-12. The son of man came to seek and save that which…
SERIES: CHRISTMAS IS JESUS CHRIST. TEXT: MATTHEW 1:21 Jesus Christ is the savior of…
MFULULIZO: JINSI YA KUISHI KATIKA UFALME WA MUNGU. SOMO: MATHAYO 6:33. Ufalme wa Mungu…