SOMO: ZABURI 90:12.
Leo ni Jumapili ya mwisho ya maka 2025. Kuna majuma 52 kila mwaka.
Mungu amakuwa mwaminifu kwa maisha yako na nyumba yako mwaka mzima.
Ujumbe wa leo unafundisha jinsi sisi Wakristo tunaweza kumaliza mwaka katika amani, shukrani, ujasiri na furaha, huku tukitembea katika hekima, utii na kujiweka mikononi kwa Mungu.
Biblia inasema:-
Basi utujulishe kuzihesabu siku zetu, tujipatie moyo wa hekima”-Zaburi 90:12.
Mungu uhesabu umri kwa siku, wala si kwa miaka kama wanadamu-Zaburi 39:4.
Mwaka huu wa 2025 umekaribia kwisha, tunahitaji kutazama nyuma kuona jinsi ulivyotumia mwaka mzima. Lakini tunapo tazama nyuma, tukawe na shukrani kwa ushindi tuliopewa na Mungu. Mapenzi ya Mungu kwetu ni kumaliza kila mwaka na kila msimu (season) bila shaka na majuto, huku tukiwa tumefungwa na rehema na neema zake na kuongozwa na hekima yake.
Majuto yanakuja kwa sababu ya kupoteza wakati, kutotii, uhusiano uliovunjika na nafasi tuliopoteza.
Pamoja na hayo yote, Biblia inatufundisha kwamba rehema za Mungu ni mpya kila ashubuhi. Neema ya Mungu inakomboa wakati uliopotea tunapojiweka katika mapenzi yake.
Hivyo, mwito wa Mungu kwetu leo, ni kumaliza mwaka bila majuto, huku tukinyenyekea chini ya mikono ya Mungu, tukiishi ka imani na kumtumaini Mungu kila siku. Pamoja na kufahamu kwamba yote yaliyotendeka kwetu yawe mazuri au mabaya, yote yalichangia mpango wa Mungu kwa maisha yetu. Hebu tutazame:-
TAMBUA REHEMA ZA MUNGU KWA MWAKA MZIMA (2025).
Mungu alidumisha maisha yako-Maombolezo 3:22-23.
Mungu alikujalia nguvu kila siku-Isaya 46:4.
Mungu alikuwa mwaminifu kwako hata wakati ulishindwa
–2 Timotheo 2:13.
Mungu alikuongoza miguu na kila hatua-Mithali 16:9.
WACHILIA MAJUTO YA MWAKA YAENDE.
Mungu ameamuru tutazame mbele-Wafilipi 3:13-14.
Mungu anarejesha wakati uliopotea-Yoeli 2:25.
Mungu anasamehe dhambi tunazotubu-Yohana 1:9.
Mungu anafanya makosa tuliyofanya kuwa somo-Warumi 8:28.
MALIZA MWAKA KATIKA UTII NA SHUKRANI.
Utii unaleta amani-Isaya 1:19.
Shukrani inalainisha mtizamo wetu-1 Wathesalonike 5:18.
Sifa na ibada inafungua mwaka vizuri-Zaburi 92:1-2.
Unyenyekevu unavutia neema ya Mungu kwetu-Yakobo 4:6.
HEKIMA YA KUPANGA MWAKA UJAO.
Hekima inafanya moyo kuwa tayari-Mithali 4:7.
Maono yanafanya njia yetu kuwa wazi-Habakuki 2:2.
MWISHO
MFULULIZO: MJUE MUNGU WAKO. SOMO: ISAYA 8:18. Mungu wetu ni YEHOVAH. Yehovah si Mungu…
SERIES: “NEARER MY GOD TO THEE.” TEXT: PSALM 42:7. Many believers settle for shallow…
SERIES: THE POWER OF PRAYER AND FASTING TEXT: ISAIAH 58:3-9 God desires that we…
MFULULIZO: MJUE MUNGU WAKO. SOMO: 1 WAFALME 20:23-28. Mabonde si mahali pa kuachwa lakini…
SERIES: NEARER MY GOD TO THEE.” TEXT: PSALM 91:1-2. The secret place is not…
SERIES: THE POWER OF PRAYER AND FASTING. TEXT: JOEL 2:12. Prayer and fasting has…