MFULULIZO: MJUE MUNGU WAKO.
SOMO: 1 WAFALME 20:23-28.
Mabonde si mahali pa kuachwa lakini ni mahali pa kumkabidhi na kukutana na Mungu. Mabonde katika maisha ni sehemu ya safari yetu ya kiroho, hapa bondeni ndipo tutaona uaminifu wa Mungu kwa kina.
Bonde katika maisha ni picha ya nyakati za maumivu, kuvunjika mioyo, kukata tamaa, nyakati za kupoteza na wakati wa kukosa hakika.
Watu wengi wanamwona Mungu wao zaidi juu ya milima ya maisha, lakini wanakosa kuona uwepo wake wanapopita katika bonde.
Mungu ni Mungu wa milimani na pia ni Mungu mabondeni!!
Majeshi ya Shamu walikosa waliposema Mungu wa Israeli ni Mungu wa milimani, lakini si Mungu wa mabondeni na chi tambarare-1 Wafalme 20:23-28. Mungu wa Israeli aliwaonyesha kwamba yeye ni Mungu wa bondeni na nchi tambarare.
Hii ni kuonyesha kwamba uwepo wa Mungu, nguvu zake na makusudi yake yako kila mahali hata wakati wa shida na dhiki za maisha.
Katika ujumbe wetu hivi leo, tutajifunza jinsi Mungu anatembea pamoja nasi katika bonde, jinsi anatupigania na kufanya bonde liwe mahali pa ufufuo na urejesho. Hebu tutazame:-
MUNGU YU PAMOJA NASI KATIKA BONDE LA MAISHA.
Mungu anatembea nasi bondeni-Zaburi 23:4.
Bondeni sio mwisho wa safari-Hosea 2:14-15.
Uwepo wa Mungu huleta ujasiri bondeni la maisha-Joshua 1:9.
Bonde inatufundisha kumtumaini Mungu zaidi-Warumi 8:28.
MUNGU ANATUPIGANIA KATIKA BONDE LA MAISHA.
Adui zako wanadharau Mungu wako unapokuwa katika bonde la maisha-1 Wafalme 20:28.
Bonde lako ndipo uwanda wa ushindi katika vita-2 Mambo ya Nyakati 20:15-17.
Mungu anatumia bonde za maisha yako kuonyesha ukuu wake-Zaburi 44:3-7.
Unaposimama wima, Mungu atajidhihirisha kwako-Kutoka 14:13-14.
MUNGU ANAREJESHA UZIMA WAKO KATIKA BONDE LA MAISHA.
Bonde ni mahali pa unabii-Ezekieli 37:1-10.
Mungu anapopumua uzima kwa chochote kilicho kufa-Ayubu 14:7-9.
Neno la Bwana lina nguvu bondeni-Isaya 55:11.
Urejesho unaonekana mahali utii unaanza katika lile bonde la mauti-Ezekieli 37:7.
MUNGU ANAONGEA KATIKA BONDE LA UAMUZI.
Mabonde yanafichua hali ya mioyo yetu-Kumbu kumbu 8:2.
Bonde ni mahali pa uamuzi-Yoeli 3:14.
Mungu anatuita kujitoa kamilifu katika bonde la maisha-Warumi 12:1-2.
Bonde la maisha inatufanya kuwa tayari kwa mlima unaokuja mbele zetu-Yakobo 1:2-4.
MWISHO
MFULULIZO: MJUE MUNGU WAKO. SOMO: ISAYA 8:18. Mungu wetu ni YEHOVAH. Yehovah si Mungu…
SERIES: “NEARER MY GOD TO THEE.” TEXT: PSALM 42:7. Many believers settle for shallow…
SERIES: THE POWER OF PRAYER AND FASTING TEXT: ISAIAH 58:3-9 God desires that we…
SERIES: NEARER MY GOD TO THEE.” TEXT: PSALM 91:1-2. The secret place is not…
SERIES: THE POWER OF PRAYER AND FASTING. TEXT: JOEL 2:12. Prayer and fasting has…
SERIES: HOW TO FULFILL YOUR DIVINE DESTINY. TEXT: JEREMIAH 1:4-12. Fulfilling divine purpose means…