MFULULIZO: MJUE MUNGU WAKO.
SOMO: ISAYA 8:18.
Mungu wetu ni YEHOVAH. Yehovah si Mungu mtupu na kimya-bali ni Mungu wa ishara na maajabu. Kutoka Mwanzo mpaka Ufunuo, Biblia inaonyesha Mungu anayejidhihirisha kwa ishara, maajabu na miujiza. Ajabu zake zinapita fahamu zote za mwanadamu.
Ishara, maajabu na miujiza ya Mungu si ya kutumbuiza mwanadamu, bali ni njia zake za kutangaza uwezo, uwepo na mapenzi yake, huku akiwatafuta watu wamjie.
Ishara na maajabu ni njia za Mungu kuingilia kati na majira ya asili, hili mwanadamu aweze kumheshimu Mungu.
Ishara na maajabu zinaleta ukombozi kwa waliomateka ya shetani, kuwaponya walio wagonjwa, kuwalisha walio na njaa, kuwatosheleza walio na mahitaji na kujenga imani kwa walio dhaifu.
Ishara, maaajabu na miujiza ni maonyesho ya Mungu asiyeonekana.
Leo, tunapotazama asili na sababu za ishara, maajabu na miujiza, tukumbuke kwamba Mungu angali Mungu wa ishara, maajabu na miujiza. Leo kama zamani uwezo wa Mungu bado pungua na mapenzi yake kujionyesha kwa uwezo na nguvu zake ni kama zamani na zaidi leo kuliko zamani. Hebu tutazame:-
MUNGU ANAONYESHA NGUVU NA UWEZO WAKE KUPITIA ISHARA, MAAJABU NA MIUJIZA.
Ishara zinaonyesha uungu wa nguvu za Mungu juu ya viumbe vyote-Kutoka 14:21-22.
Maajabu yanaonyesha mamlaka ya Mungu juu ya magonjwa na mauti-Yohana 11:43-44.
Mungu anatumia ishara kudhibitisha watumishi wake-Matendo 2:22.
Ishara ni sehemu ya Agano la Mungu na watu wake-Marko 16:17-18.
ISHARA NA MAAJABU YANAWAVUTA WATU KWA WOKOVU.
Ishara zinadhibitisha habari njema na Injili-Waebrania 2:4.
Ishara zinavunja kutoamini na pingamizi kwa Injili-Matendo 8:6-8.
Maajabu yanafungua milango ya kuhubiri Injili duniani-Matendo 3:6-10.
Ishara zinawarudisha watu wengi kwa Mungu-Yohana 2:11.
MUNGU ANGALI ANAFANYA ISHARA, MIUJIZA NA MAAJABU LEO.
Yesu Kristo bado ni yule jana, leo na milele-Waebrania 13:8.
Mungu anaamkia panapo matarajio ya imani-Mathayo 9:29.
Ishara zinawafuata wanaoamini-Marko 16:17-18.
Kanisa ni jukwaa na uwanda wa maonyesho ya uwezo na uwepo wa Mungu-1 Wakorintho 2:45.
WAUMINI WANAHITAJI KUMFUATA MUNGU LAKINI SI KUTAFUTA MIUJIZA, ISHARA NA MAAJABU.
Usikimbilie miujiza-lakini kimbilia Mungu wa miujiza-Mathayo 6:33.
Ishara zinadhibitisha neno, lakini si kuchukua mahali pa neno-Yohana 4:48.
Tembea katika utakatifu na utii upate kubeba nguvu za Mungu-Matendo 5:32.
Ishi maisha ya unyenyekevu na mpe Mungu utukufu wote-Matendo 3:12-13.
MWISHO
SERIES: “NEARER MY GOD TO THEE.” TEXT: PSALM 42:7. Many believers settle for shallow…
SERIES: THE POWER OF PRAYER AND FASTING TEXT: ISAIAH 58:3-9 God desires that we…
MFULULIZO: MJUE MUNGU WAKO. SOMO: 1 WAFALME 20:23-28. Mabonde si mahali pa kuachwa lakini…
SERIES: NEARER MY GOD TO THEE.” TEXT: PSALM 91:1-2. The secret place is not…
SERIES: THE POWER OF PRAYER AND FASTING. TEXT: JOEL 2:12. Prayer and fasting has…
SERIES: HOW TO FULFILL YOUR DIVINE DESTINY. TEXT: JEREMIAH 1:4-12. Fulfilling divine purpose means…