Categories: Swahili Service

MUNGU WA MILIMA

MFULULIZO: MJUE MUNGU WAKO.

SOMO: ZABURI 121:1-2, 1 WAFALME 20:23-28.

 

“Mungu wa milima” si Mungu wa milima kigeographia, lakini Mungu wa milima kiroho. Katika Biblia milima inawakilisha changamoto, Ufunuo wa Mungu nyakati za kujitakasa na mahali pa kumkabidhi Mungu. Katika Biblia milima imetumika kama mahali pa mwanadamu kukutana na Mungu. Katika Mlima Sayuni, kutoka mlima wa Moria mpaka mlima wa Mzeutuni Mungu ametumia milima kama mahali pa kujivua kwa mwanadamu. Milima ni mahali palipoinuka juu zaidi ya mabonde, mahali vikwazo na vidhibiti vya mwanadamu vinabadilishwa kuwa mahali pa Ufunuo wa Mungu.

Katika 1 Wafalme 20:23-28, majeshi ya Shamu waliamini kimakosa kwamba Mungu wa Israeli ni Mungu wa milima pekee, kwamba Mungu wa Israeli hawezi vita vya nchi tambarale na mabonde!!

Lakini Yehova alijidhiirisha kwamba yeye ni Mungu wa milima, nchi tambarare na mabondeni, Yehova ni Mungu kila mahali.

Tunapojifunza somo hili tutaona jinsi Mungu anatumia milima katika maisha yetu kudhihirisha nguvu na uwezo wake, kudhibitisha imani yetu na kudumisha hatima zetu. Hebu tutazame:-

MUNGU ANAJIDHIHIRISHA MLIMANI.

  • Milima ni mahali pa Mungu kujidhihirisha na kujifunua kwa watu wake.

Milima ni mahali Mungu amechagua kujidhihirisha-Kutoka 19:16-20.

  • Mlima Sinai, Mungu alishuka katika moto, moshi na ghurumo nyingi kujidhihirisha kwa Israeli.

Mlima ni ishara ya kujitenga kwa Mungu-Isaya 2:2-3.

  • Mungu anawaita watu wake waje mlimani wapate kumjua zaidi.

Juu ya mlima Mungu anaongea vyema zaidi-Kutoka 20:1.

  • Amri kumi za Mungu zilitolewa juu ya mlima Sinai.
  • Sauti ya Mungu ilisikika vizuri zaidi kutoka mlimani.

Mlima ni mahali pa kuwa karibu na Mungu zaidi-Mathayo 17:1-2.

  • Yesu Kristo alibadilishwa juu ya mlima, wanafunzi wake waliona utukufu wake.
  • Musa naye, alionana na Mungu uso kwa uso juu ya mlima Sinai-Kutoka 34:29-35.

MUNGU ANATOA JUU YA MLIMA.

  • Milima ni ishara ya mahali Mungu anatoa na kutosheleza watu wake kwa kila hitaji.
  • Milima ni mahali Mungu anabadilishana dhabihu (substitution).

Mungu anajaribu imani kabla kutoa-Mwanzo 22:1-2.

  • Ibrahimu aliambiwa kumtoa mwana wake wa pekee (Isaka) mlimani Moria. Hii ilikuwa jaribu kubwa ya imani ya Ibrahimu.
  • Hii ilikuwa jaribu ya imani na kujisalimisha.

Mungu atatoa juu ya mlima-Mwanzo 22:14.

  • Mungu alitoa kondoo badala ya Isaka, Mungu alijidhihirisha kuwa Yehova Jire.

Kutoa kunakuja baada ya utii-Mwanzo 22:12-13.

  • Mungu atatoa kwako anapoona utii kamili.

Mungu anatoa kile huwezi kuona na macho yako mpaka utakapofika pale-Mwanzo 22:8.

  • Imani itakupandisha milimani, utii nao unafungua utoshelevu wa Mungu.

MUNGU HUBADILISHA WATU MLIMANI.

  • Mlimani ni mahali mioyo inabadilishwa, maono yanapatikana na kitambulisho kinabadilika na kudhibitika.

Kubadilika kunakuja panapo uwepo wa Mungu-Mathayo 17:1-8.

  • Yesu alipobadilishwa juu ya mlima, wanafunzi wake walimtambua.

Milima inageuza maono yetu-Kutoka 34:29.

  • Musa alibadilishwa juu ya mlima Sinai, uso wake ulijaa utukufu wa Mungu.

Tunapokutana na Mungu maisha yetu yanabadilika kabisa-Isaya 6:1-8.

  • Isaya alikutana na Mungu juu ya mlima katika roho.

Mlima utakuinua juu zaidi ya yote na vikwazo vyote-Marko 6:46.

  • Yesu Kristo alipanda milimani kuomba mbali na kelele za watu.
  • Eliya naye juu ya mlima Herobu alisikia sauti ya Mungu-1 Wafalme 19:8-12.

MUNGU ANAWAPA WATU WAKE USHINDI KUTOKA MLIMA.

  • Mungu wa mlima huwapa watu wake nguvu na ushindi.

Mungu hajakabwa na hali na mahali-1 Wafalme 20:28.

  • Mungu ni Mungu wa milima na mabonde.
  • Nguvu za Mungu ziko kila mahali.

Milimani ni mahali pa vita vya kiroho-2 Nyakati 20:20.

  • Mungu anapatiana mwelekeo wa nguvu kwa wale wamfuatao.

Ibada juu ya mlima anaongoza kwa kupenya-Zaburi 121:1-2.

  • Msaada wetu unatoka kwa Mungu aliye juu zaidi ya milima yote.

Kutoka juu ya milima tunaona vyema zaidi kuliko bondeni-Kumbu kumbu 34:1-4.

  • Musa alitazama nchi ya ahadi kutoka mlima wa Pisga-kuonyesha kwamba tunaona vyema zaidi juu ya mlima.

MWISHO

  • Mungu wa milima ni Mungu wa kuwapandisha watu wake, Mungu wa Ufunuo, kutosheleza na kutoa. Mungu wa kuwapandisha watu.
  • Mungu wa milimani huwapa watu wake nguvu mpya na kuwapa utukufu wake.
  • Lakini Mungu wa milimani pia ndiye Mungu wa mabondeni na nchi tambarale. Huyu ni Mungu asiye na mipaka.
  • Tunahitaji kupanda milima yote itakayo jitokeza mbele ya maisha yetu, huku tukifahamu kwamba Mungu wetu ni Mungu wa milimani.
  • Milima ni changamoto zote tutakazopitia katika mwaka 2026.
  • Hatima yako imo katika Mungu wa milimani na mabondeni.
The following two tabs change content below.
Rev, Dr. Willy Mutiso is the Senior Pastor at First Baptist Athiriver. He is widely known for his practical and dynamic teaching style which helps people apply the timeless truths of Scripture to their everyday lives.

Latest posts by Rev, DR. Willy Mutiso (see all)

Rev, DR. Willy Mutiso

Rev, Dr. Willy Mutiso is the Senior Pastor at First Baptist Athiriver. He is widely known for his practical and dynamic teaching style which helps people apply the timeless truths of Scripture to their everyday lives.

Share
Published by
Rev, DR. Willy Mutiso

Recent Posts

MUNGU WA ISHARA NA MAAJABU

MFULULIZO: MJUE MUNGU WAKO. SOMO: ISAYA 8:18.   Mungu wetu ni YEHOVAH. Yehovah si Mungu…

3 hours ago

DEEP CALLS TO DEEP-A JOURNEY INTO GOD

SERIES: “NEARER MY GOD TO THEE.” TEXT: PSALM 42:7.   Many believers settle for shallow…

5 hours ago

THE KIND OF FAST GOD LOVES

SERIES: THE POWER OF PRAYER AND FASTING  TEXT: ISAIAH 58:3-9   God desires that we…

7 hours ago

MUNGU NI MUNGU WA MABONDENI

MFULULIZO: MJUE MUNGU WAKO. SOMO: 1 WAFALME 20:23-28.   Mabonde si mahali pa kuachwa lakini…

1 week ago

THE SECRET PLACE: FINDING GOD’S PRESENCE

SERIES: NEARER MY GOD TO THEE.” TEXT: PSALM 91:1-2.   The secret place is not…

1 week ago

HOW FASTING MOVED MOUNTAINS

SERIES: THE POWER OF PRAYER AND FASTING. TEXT: JOEL 2:12.   Prayer and fasting has…

1 week ago