MFULULIZO: MJUE MUNGU WAKO.
SOMO: MWANZO 7:16.
Mungu anapomfungia mtu, anafungia nje mauti, hatari zote, tauni na uaribifu wote. Katika mwaka huu wa 2026, sisi hatuhesabu ulinzi kutoka kwa mwanadamu au kutegemea nguvu za mwanadamu-Tunamlilia Mungu Bwana wetu pekee atupe ulinzi wake. Tunategemea nguvu zake za kutufungia-Mwanzo 7:16.
“Na walioingia,waliingia mume na mke na kila kitu chenye mwili, kama vile alivyomwamuru Mungu, Bwana akimfungia.”
Kila mtu anapenda kuwa salama-Usalama kutokana na maovu, hatari, uaribifu na dhoruba za maisha.
Usalama ni hitaji la msingi kwa kila mmoja wetu, lakini katika dunia inayojaa dhoruba na ubaya na dhambi, ulinzi wa mwili huwezi kutosha. Hata ingawa tunafunga nyumba zetu, tunaweka CCTV, na kujilinda kwa magonjwa, lakini mabaya na maovu yanatupata.
Ukweli ni kwamba mipango ya mwanadamu kujilinda haitoshi. Lakini ulinzi wa Mungu ni kamilifu.
Katika Mwanzo 6, Nuhu alimtii Mungu kujenga ile safina. Nuhu aliyafuata maagizo ya Mungu, alitumia vifaa vyote kama jinsi yaliyokuwa maagizo ya Mungu, lakini baada ya yote kutendeka, Mungu alifanya jambo la ajabu kuu-Mwanzo 7:16, “Bwana akamfungia.”
Kifungu hiki cha maandiko kina maana fiche, kwamba usalama na ulinzi wa kweli hautoki tu katika kumjua Mungu na kumtii, lakini ulinzi wa kweli unatoka kwa Mungu.
Safina ilikuwa salama si tu sababu ilijengwa vizuri lakini kwa sababu Mungu mwenyewe alimfungia Nuhu ndani ya lile safina.
“Bwana alimfungia” haikuwa kufungiwa ki-asili lakini Maanake ni kwamba BWANA alimfungia Nuhi kiroho,,mbali na hukumu, hatari na uaribifu.
Mungu aliye “Mfungia” Nuhu ni yeye yule anaye wafungia watu wake leo.
Mungu anapokufungia, basi, amefungia nje yako mauti, hatari na uaribifu. Katika mwaka huu wa 2026, hatutegemei mbinu, mipango na nguvu za mwanadamu, tunamlilia Mungu wa ulinzi atufungie ndani. Hebu tutazame:-
KUFUNGULIWA NA MUNGU, NI MUNGU KUJITOA KUKULINDA WEWE.
Mungu hatumi watu kukulinda-Zaburi 121:3-4.
Mhuri wake una nguvu zaidi kuliko nguvu za mwanadamu-Mhubiri 9:11.
Ulinzi wa Mungu ni kamilifu na tosha-Ayubu 1:10.
Mungu anapokufungia-hakuna kitu chochote kinaweza kuingia pasipo kibali cha Mungu-Ufunuo 3:7.
ULINZI WA MUNGU UNAFUNGIA NJE GHARIKA NA MAFURIKO YA ADUI.
Leo hii kuna mkondo na mafuriko ya uovu duniani-Isaya 59:19.
Mungu anajua jinsi ya kuwalinda watu wake katikati ya hukumu-2 Petro 2:9.
Ulinzi wa Mungu si kwa mwili pekee, bali ni pamoja na nafsi, roho na hisia-Zaburi 91:5-6.
“Kufungiwa ndani” na Mungu Maanake ni kuzingirwa na uwepo wa Mungu-Zakaria 2:5.
MUNGU ANAPOKUFUNGIA NDANI ANAFUNGIA NJE KULA NGUVU ZA GIZA.
Mungu anajua kilio cha kufungia ndani na kile cha kufungia nje-Zaburi 34:7.
Kufungiwa ndani Maanake ni kufunikwa hata husipofahamu-Zaburi 121:7-8.
Mungu anapokulinda hakuna mpango wako utakao kosa kustawi-Isaya 46:10.
KUFUNGIWA NDANI NA MUNGU, KUNAHITAJI UTII NA IMANI.
Nuhu alitii maagizo, akajenga lile safina kulingana na maagizo-Mwanzo 6:22.
Kulindwa na Mungu ni dhawabu ya kutembea na Mungu-Mwanzo 6:9.
Ni lazima kudumu katika uwepo wa Mungu hili tupokee ulinzi wake-Ruthu 2:12.
ULINZI WA MUNGU NI KWA VIZAZI KWA VIZAZI NA ULINZI WA MUNGU UNAWEZA KUPEANWA.
Mungu anapokufungia ndani, anakufungia pamoja na nyumba yako-Mwanzo 7:1.
Ulinzi wa Mungu unawafunika watoto wako hata wakati umekufa-Zaburi 103:17.
Ulinzi wa maagano unawafikia wote, uzao wako wa kiroho na uzao wa mwili-Matendo 2:39.
MWISHO
SERIES: HOLINESS- GOD’S WAY TO GREATNESS TEXT: 1st PETER 1:15-17 Holiness is the character…
SERIES: HOW TO FULFILL YOUR DIVINE DESTINY. TEXT: MATTHEW 2:1-2. Every person carries a…
MFULULIZO: MJUE MUNGU WAKO. SOMO: ISAYA 8:18. Mungu wetu ni YEHOVAH. Yehovah si Mungu…
SERIES: “NEARER MY GOD TO THEE.” TEXT: PSALM 42:7. Many believers settle for shallow…
SERIES: THE POWER OF PRAYER AND FASTING TEXT: ISAIAH 58:3-9 God desires that we…
SERIES: HOW TO FULFILL YOUR DIVINE DESTINY. TEXT: JOHN 10:10, ISAIAH 45:2 Guarding your…