ISAYA 1:18

UTANGULIZI

Nabii Isaya alitumika katika wakati kama  wakati tulionao hapa kwetu Kenya. Inchi ya Israeli ilikuwa imemwacha Mungu na njia zake. Watu wa Mungu walikuwa wanaishi katika dhambi na ibada za sanamu.

(v.2) watu walikuwa wamemuasi Mungu.

V.3: Israeli walikuwa wamemkataa Mungu, kwa kweli walikuwa wameshidwa akili na wanyama.

V.4: Walichukua mzigo wa dhambi na uovu.

V.5: Walikuwa wagonjwa wa moyo na kuzimia

V.7-8: Ubaya ulienea kila mahali.

V.9-10: Walikuwa kama Sodoma na Gomora.

V.11-15: Ibada zao zilikuwa chukizo kwa Mungu.

V.9: Mabaki wachache ndio walibaki Israeli yote.

Watu hawawezi kumtafuta Mungu kwa nguvu zao wenyewe. (I Yohana 4:19, Waefeso 2:1-3, Luka 19:10).

Bwana anawaalika watu wa Israeli wamnjie. Hivi leo, Mungu anawaalika, wenye dhambi, wamjie wapate utakaso.

Hebu tuone:-

 

I.  TATIZO YA MWALIKO HUU.

  1. Haya, njoni tusemezane asema Bwana.
  • Mwaliko huu ni Amri kutoka kwa Mungu.
  • Mungu anafahamu mioyo yetu, anajua dhambi zetu.
  • Neema na Rehema zake zipo kwa wote wamnjiao.
  1. Mungu anafahamu dhambi zetu, anajua kwamba sisi tu wenye dhambi, waovu na wenye kupungukiwa sana. (Ufunuo 22:17, Yohana 7:37, Mathayo 11:28)
  2. Mungu anafahamu hali ya mioyo yetu kuliko sisi wenyewe. (Warumi 5:6-8)

II.  HARAKA ZA MWALIKO HUU.

  1. Amri ya Mungu ni tumjie sasa, bila kuchelewa.
  • Mungu anaona njia zetu na muelekeo wa mioyo yetu.
  1. Hivyo ndivyo ilivyo kwa wote wasio haki mbele zake. (II Wathesa.1:8-9, Zaburi 9:17, Mathayo 13:42, Ufunuo 14:11)
  2. Kama umeokoka, kwenda mbali na Mungu kunaleta nidhamu zake (Waeb.12:6-11)
  3. Mungu anajua jinsi mambo yatakuwa mbaya zaidi kwa wemye dhambi. (Mwanzo 6:3, Mithali 27:1, II Wakor.6:2)

III. URAFIKI WA MWALIKO HUU.

  1. “Haya, njoni tusemezane, Asema Bwana.”
  • Bwana anasema tusawazishe mambo ya mioyo yetu – Tusemezane.
  1. Mungu anawaita watu binafsi, wala si kwa jumla. (Yohana 16:7-13)
  2. Je, umesikia mwaliko huu wa Mungu kibinafsi?

 

IV.  AJABU YA MWALIKO HUU.

  1. Ahadi za Mungu kwa Israeli, ikiwa watamjia ni kwamba dhambi zao zijapokuwa nyekundu sana, zitakua nyeupe kama theluji.
  2. Mwaliko huu ungalipo leo. (Isaya 64:6)
  3. Je, wewe una hakika dhambi zako zime samehewa?

 

MWISHO

¨ Bwana anakuita leo, sikia mwito na mwaliko wake.

¨ Bwana anakuita nje ya korti kusemezana leo.

¨ Wamebarikiwa wanao tii sauti ya Bwana anapowaita.

 

The following two tabs change content below.
Rev, Dr. Willy Mutiso is the Senior Pastor at First Baptist Athiriver. He is widely known for his practical and dynamic teaching style which helps people apply the timeless truths of Scripture to their everyday lives.

Latest posts by Rev, DR. Willy Mutiso (see all)

Rev, DR. Willy Mutiso

Rev, Dr. Willy Mutiso is the Senior Pastor at First Baptist Athiriver. He is widely known for his practical and dynamic teaching style which helps people apply the timeless truths of Scripture to their everyday lives.

Share
Published by
Rev, DR. Willy Mutiso

Recent Posts

DAMU YA UTAKASO.

MFULULIZO: AGANO LA UTAKASO. SOMO: KUTOKA 12:12-13.   Damu ya Yesu Kristo ndiyo mhuri wa…

11 hours ago

KEY TO DIVINE SPEED.

SERIES: SUPERNATURAL ADVANCEMENT. TEXT: HABAKKUK 3:19.   The journey of fulfilling your destiny does not…

13 hours ago

BE YE THANKFUL TO GOD.

SERIES: THROUGH THE BOOK OF COLOSSIANS. TEXT: COLOSSIANS 3:15   Thankfulness is a great attitude…

15 hours ago

LEVELS OF THE ANOINTING.

SERIES: THE ANOINTING. TEXT: EZEKIEL 47:1-5   There are levels of the anointing and each…

4 days ago

UMETAKASWA KUPOKEA KIBALI.

MFULULIZO: AGANO LA UTAKASO. SOMO: ESTA 2:15-18.   Kibali cha Mungu ndicho kinacho watenga watoto…

1 week ago

THE GOD WHO SHIFTS THE HEAVENS IN YOUR FAVOR.

SERIES: THE GOD WHO NEVER FAILS. TEXT: HAGGAI 2:6-9.   God has the power to…

1 week ago