Categories: Swahili Service

NJIA YA KWENDA MSALABANI.

MFULULIZO: PASAKA

SOMO: YOHANA 12:9-19

 

Yesu Kristo alianza safari ya kwenda msalabani kwa kuingia Yerusalemu. Njia hii ya kwenda msalabani ilikuwa ni njia ya huzunu na mateso mengi lakini Yesu Kristo alichagua kuipitia njia hiyo. Watu wengi walimlaki Kristo, huku wakitoa mavazi yao na kutandaza matawi ya mitende. Waliimba wimbo wa Hosana, hosanna “tuokoe sasa.” Unabii wa Zakaria 9:9, ulitimia siku hii ya Jumapili ya mitende, miaka 2000 iliyopita. Hebu tujifunze:-

NJIA YA KWENDA MSALABANI ILIKUWA NJIA YA HATIMA-Yohana 12:12-13.

Yesu Kristo alikuja duniani kuokoa sasa wakati huo ulifika.

  • 13, Neno “Hosana” Maanake ni “okoa sasa.”
  • Watu wote walikuwa tayari kwa ukombozi.
  • Yesu Kristo alikuja kuokoa watu na dhambi zao-lakini watu walitarajia ukombozi wa kisiasa, ukombozi kutoka kwa utawala wa Roma.

Watu waliamini sana Yesu Kristo alitoka kwa Mungu.

  • Yesu Kristo alikuwa chaguo la wote kuwa “masihi” alitimiza yote ya unabii-Zakaria 9:9

NJIA YA KWENDA MSALABANI ILIKUWA NJIA YA KUJITOA-Yohana 12:14-15.

Kule kuingia Yerusalemu kulitangaza kujitoa kwake kwa kazi iliyokuwa mbele zake Mwokozi.

  • Lakini safari ya kwenda msalabani haikuanza mle Bethania, safari hii ilianza milele.
  • Safari hii ya kwenda msalabani ilianza Edeni, wazazi wetu walipofanya dhambi ya kwanza.
  • Katika milele hata kabla kuumbwa kwa mbingu na nchi.
  • Safari ya Yesu Kristo kutuokoa ilianza milele.

Kuja kwake Yesu Kristo duniani kulikuwa ni kujitoa kwake kwa Baba yake.

  • Watu walihitaji mfalme sana, kiasi walitaka sana kumlazimisha Yesu Kristo kuwa mfalme wao.
  • Watu hawa hawakutaka ukombozi kutoka dhambi lakini ukombozi kutoka kwa utumwa wa Roma.
  • Watu hawa hawakutaka kufanya mapenzi ya Mungu lakini ushindi juu ya Roma.
  • Watu walishangaa badala ya Yesu kuingia Yerusalemu juu ya farasi ya vita, aliingia Yerusalemu juu ya punda, ishara ya amani-Marko 10:45.

NJIA YA KWENDA MSALABANI ILIKUWA NJIA YA UVUMBUZI-Yohana 12:16

Watu hawa walitambua kwamba mawazo yao juu ya masihi yalikuwa makosa.

  • Walimsalimia Kristo kama mfalme wao, lakini hawakutambua ufalme wake ulikuwa ufalme gani.
  • Hawakuelewa ufalme wa Kristo juu ya maisha yao.

Wanafunzi wa Yesu Kristo na wao walitambua mpango wa Mungu kwa ulimwengu.

  • Wanafunzi wa Yesu Kristo hawakutambua jinsi ya kazi na shabaha ya Yesu Kristo mpaka kufufuka kwake.

NJIA YA KWENDA MSALABANI ILIKUWA NJIA YA UKOMBOZI-Yohana 12:17-19.

  • Njia aliyochukua Yesu Kristo ilikuwa njia ya wokovu kwa watu wote.
  • Yesu Kristo alijua kwamba ni lazima kufa ili wote wapate uzima wa milele.
  1. Hii ilikuwa njia ya ukombozi ambayo shetani hangeweza kuzuia.
  • Watu wote walijitokeza kumpokea Yesu Kristo Yerusalemu kwa ushindi mwingi zaidi.

MWISHO

  • Jumapili ya mitende ilikuwa ushindi mkuu kwa maana Yesu Kristo alikuwa anaenda msalabani kwa ajili yetu.
  • Hakuna mtu, au shetani aliyeweza kumzuia Kristo kwenda msalabani.
  • Yesu Kristo alikuja duniani kutufia, tupate kuokoka.
The following two tabs change content below.
Rev, Dr. Willy Mutiso is the Senior Pastor at First Baptist Athiriver. He is widely known for his practical and dynamic teaching style which helps people apply the timeless truths of Scripture to their everyday lives.

Latest posts by Rev, DR. Willy Mutiso (see all)

Rev, DR. Willy Mutiso

Rev, Dr. Willy Mutiso is the Senior Pastor at First Baptist Athiriver. He is widely known for his practical and dynamic teaching style which helps people apply the timeless truths of Scripture to their everyday lives.

Share
Published by
Rev, DR. Willy Mutiso

Recent Posts

DAMU YA UTAKASO.

MFULULIZO: AGANO LA UTAKASO. SOMO: KUTOKA 12:12-13.   Damu ya Yesu Kristo ndiyo mhuri wa…

2 days ago

KEY TO DIVINE SPEED.

SERIES: SUPERNATURAL ADVANCEMENT. TEXT: HABAKKUK 3:19.   The journey of fulfilling your destiny does not…

2 days ago

BE YE THANKFUL TO GOD.

SERIES: THROUGH THE BOOK OF COLOSSIANS. TEXT: COLOSSIANS 3:15   Thankfulness is a great attitude…

2 days ago

LEVELS OF THE ANOINTING.

SERIES: THE ANOINTING. TEXT: EZEKIEL 47:1-5   There are levels of the anointing and each…

6 days ago

UMETAKASWA KUPOKEA KIBALI.

MFULULIZO: AGANO LA UTAKASO. SOMO: ESTA 2:15-18.   Kibali cha Mungu ndicho kinacho watenga watoto…

1 week ago

THE GOD WHO SHIFTS THE HEAVENS IN YOUR FAVOR.

SERIES: THE GOD WHO NEVER FAILS. TEXT: HAGGAI 2:6-9.   God has the power to…

1 week ago