Categories: Swahili Service

URITHI WETU NI WA MILELE

MFULILIZO: URITHI USIOHARIBIKA MILELE

SOMO:   I PETER 1:1-5

Je,Nanga ya kushika wakati wa majaribio na mateso katika maisha yetu ni nini?Je imani yako  ikoje wakati maisha yamekuwa magumu sana? Leo twajifunza kifunguo cha kustahimili wakati wa shida. Kumbuka uridhi wetu katika Yesu Kristo ni wa milele.

Petro aliandika kwa kanisa lililokuwa katika mateso, kuchukiwa na kukataliwa. Tarehe 19 Julai 64 A.D.  Mji wa Roma uliwaka moto mkuu sana. Baada ya siku tatu moto huo ulimaliza Roma yote! Watu wa Roma waliamini  kwamba  mfalme, hau Kaisari Nero ,niyeye aliwakisha  moto huo. Niro alipendezwa sana na moto huo kiasi alicheza kinanda  chake moto ulipoendelea!!.

Lakini Kaisari Niro alifitini kwamba ni wakristo waliwakisha Roma moto huo!!.Wakristo walichukiwa  kwa sababu wengi walikuwa wayahudi,na kwa sababu wakristo walikataa kuabudu mfalme Niro yaani (Emperor Worship). Pia kwa sababu  walitangaza kwamba siku moja dunia itawaka moto, Niro alifitini.

Hivyo mateso na dhihaka, juu ya wakristo ilianza Roma, hivyo wakristo wengi wakachomwa moto, lakini wengine walikimbia mbali na kutawanyika katika mataifa ya Asia.

Mtume Petro anawaandikia kuwafariji huku akiwakumbusha wao ni wageni duniani, Nyumbani  kwao ni Mbinguni, wao ni watoto wa Mungu na pia wao ni mawe hai, taifa takatifu na makuhani watakatifu, mali ya    Mungu aliye hai. Petro anawajulisha kwamba wakamsifu Mungu katika majaribu yao.(1petro 1:3-5). Neno la katikati katika waraka huu ni URIDHI. Uridhi ni kile unachopokea kutoka kwa baba kama zawadi hau dhawabu kwa sababu wewe ni mzaliwa katika nyumba ya Baba.

Hebu na tuone:

I.  JE,URIDHI WETU KATIKA BWANA NI NINI?

  • Katika Agano la kale (O.T) Mungu aliahidi uridhi wa inchi hapa duniani.
  • Ahadi hio ilipewa Ibrahimu.
  • Wana wa Israeli waligoja sana, baadaye walipokea uridhi na Ahadi yao kupitia Joshua.
  • Lakini sisi tuliookoka tumeahidiwa uridhi wa kiroho, Mbinguni. (1 Petro 1:5).
  • Tunao wokovu wa milele ,wokovu ulio tayari kufuniliwa wakati wa mwisho.
  • Wokovu ni aina tatu:
  1. Wokovu uliopita (Past Salvation) Matendo 16:31, Warumi 10:9)
  • Tuliokolewa wakati tulipo mpokea Yesu Kristo
  1. Wokovu wa sasa (Present Salvation).
  • Tunaendelea kuokolewa kila saa(I Yohana 1:9, Wafilipi 2:12)
  • Tunaendelea kuokolewa, kukombolewa na damu ya Kristo inaendelea kutusafisha kila saa.
  1. Wokovu unaokuja (Future Salvation).
  • Tunaokolewa kabisa, kukombolewa kutoka kwa dhambi na hukumu. Huu wokovu unaokuja ndio uridhi wa milele. (Warumi 13:11,           Waebrania 1:14).

II.  KIINI CHA URIDHI WETU. (1 PETRO 1:3)

  1. Kiini cha uridhi wetu ni Mungu Baba, Baba wa Mwokozi wetu YESU KRISTO.
  • Mungu Baba ametuchangua kuokolewa na kupokea wokovu wa milele,yaani uridhi wa milele.
  1. Sababu ya Mwito wetu(1 Petro 1:3).
  • Rehema ya Mungu imetuchagua .(Tito 3:5).
  • Rehema ni nini? (Waefeso 2:4-5). Tulikuwa katika shida, maskini (Marko 10-Bartimayo).
  • Rehema ya Mungu ni nyingi zaidi (Kutoka 34:6, Zaburi 108:4, Mika 7:18, Maombolezo 3:22, Warumi 9:15, II Wakorintho 1:3)

III. JE, TUNATEKELEZA URITHI HUU WA MILELE AJE?

  • Mungu alitufanya kuzaliwa mara ya pili
  • Hili tubandilishwe, Mungu alituzaa upya katika Kristo (Yeremia 13:23, Zaburi 51:5, II Wakorintho 5:17, Waefeso 2:3, I Thess 1:10)
  • Unapomjua Kristo na kuweka Imani yako ndani yake, kunamabandiliko, kuzaliwa upya (I Petro 1:23, Yohana 3:3, 14-15, Hesabu 21)
  • Matokeo ya kuokoka, kuzaliwa upya ni “tumaini lililo hai” (I Petro 1:3)
  • Tumaini la dunia hii ni tumaini linalokufa (I Wakorintho 15:19)
  • Mauti inakata matumaini yote, lakini tumaini letu liko hai yaani Kristo Yesu. (2 Petro 3:13)

IV.  JE, KITU GANI KIMETUPATIA TUMAINI LA MILELE? (I PETRO 1:3)

  • Tumepokea urithi wa milele kwa njia ya kuzaliwa upya.
  • Kwa kuzaliwa mara ya pili tumepata tumaini ya milele. Tumaini letu limejengwa juu ya kufufuka kwa Kristo kutoka kwa wafu!! (Yohana 14:19)
  • Hivyo tunao urithi wa milele, kutoka kwa Mungu Baba, kwa sababu ya rehema yake, kupitia kuzaliwa mara ya pili.

MWISHO

  • Hata chochote kifanyike, majaribu yaje, tunao tumaini ya milele, tunao urithi wa milele mbinguni.
  • Je, umeokoka? Furahi katika majaribu na mangumu unayopitia, tunayo tumaini la milele. Hivyo tumsifu Mungu siku zote.
The following two tabs change content below.
Rev, Dr. Willy Mutiso is the Senior Pastor at First Baptist Athiriver. He is widely known for his practical and dynamic teaching style which helps people apply the timeless truths of Scripture to their everyday lives.

Latest posts by Rev, DR. Willy Mutiso (see all)

Rev, DR. Willy Mutiso

Rev, Dr. Willy Mutiso is the Senior Pastor at First Baptist Athiriver. He is widely known for his practical and dynamic teaching style which helps people apply the timeless truths of Scripture to their everyday lives.

Recent Posts

CHRISTMAS: THE BIRTH THAT BROKE EVERY BONDAGE

TEXT: LUKE 2:1-14.   The birth of Jesus Christ shattered spiritual, social and eternal barriers,…

1 day ago

CHRISTMAS: WHY DID CHRIST COME?

TEXT: JOHN 3:16-17.   Christmas unveils the divine mission behind the birth of Jesus Christ;…

2 days ago

KRISMASI MAANAKE NI FURAHA KWA DUNIA YA DHIKI NA SHIDA

MFULULIZO: KRISMASI NI KUFUNULIWA KWA YESU KRISTO.  SOMO: LUKA 2:8-14.   Krismasi inafunua jibu la…

5 days ago

CHRISTMAS IS WHEN HEAVEN CAME DOWN TO EARTH.

SERIES: CHRISTMAS IS CHRIST. TEXT: JOHN 1:1-14.   Christmas is the divine moment when God…

5 days ago

FOR GOD SO LOVED THE WORLD

TEXT: ISAIAH 53:1-12.   The son of man came to seek and save that which…

5 days ago

JESUS OUR SAVIOR

SERIES: CHRISTMAS IS JESUS CHRIST. TEXT: MATTHEW 1:21   Jesus Christ is the savior of…

2 weeks ago