Categories: Swahili Service

URITHI WETU NI WA MILELE

MFULILIZO: URITHI USIOHARIBIKA MILELE

SOMO:   I PETER 1:1-5

Je,Nanga ya kushika wakati wa majaribio na mateso katika maisha yetu ni nini?Je imani yako  ikoje wakati maisha yamekuwa magumu sana? Leo twajifunza kifunguo cha kustahimili wakati wa shida. Kumbuka uridhi wetu katika Yesu Kristo ni wa milele.

Petro aliandika kwa kanisa lililokuwa katika mateso, kuchukiwa na kukataliwa. Tarehe 19 Julai 64 A.D.  Mji wa Roma uliwaka moto mkuu sana. Baada ya siku tatu moto huo ulimaliza Roma yote! Watu wa Roma waliamini  kwamba  mfalme, hau Kaisari Nero ,niyeye aliwakisha  moto huo. Niro alipendezwa sana na moto huo kiasi alicheza kinanda  chake moto ulipoendelea!!.

Lakini Kaisari Niro alifitini kwamba ni wakristo waliwakisha Roma moto huo!!.Wakristo walichukiwa  kwa sababu wengi walikuwa wayahudi,na kwa sababu wakristo walikataa kuabudu mfalme Niro yaani (Emperor Worship). Pia kwa sababu  walitangaza kwamba siku moja dunia itawaka moto, Niro alifitini.

Hivyo mateso na dhihaka, juu ya wakristo ilianza Roma, hivyo wakristo wengi wakachomwa moto, lakini wengine walikimbia mbali na kutawanyika katika mataifa ya Asia.

Mtume Petro anawaandikia kuwafariji huku akiwakumbusha wao ni wageni duniani, Nyumbani  kwao ni Mbinguni, wao ni watoto wa Mungu na pia wao ni mawe hai, taifa takatifu na makuhani watakatifu, mali ya    Mungu aliye hai. Petro anawajulisha kwamba wakamsifu Mungu katika majaribu yao.(1petro 1:3-5). Neno la katikati katika waraka huu ni URIDHI. Uridhi ni kile unachopokea kutoka kwa baba kama zawadi hau dhawabu kwa sababu wewe ni mzaliwa katika nyumba ya Baba.

Hebu na tuone:

I.  JE,URIDHI WETU KATIKA BWANA NI NINI?

  • Katika Agano la kale (O.T) Mungu aliahidi uridhi wa inchi hapa duniani.
  • Ahadi hio ilipewa Ibrahimu.
  • Wana wa Israeli waligoja sana, baadaye walipokea uridhi na Ahadi yao kupitia Joshua.
  • Lakini sisi tuliookoka tumeahidiwa uridhi wa kiroho, Mbinguni. (1 Petro 1:5).
  • Tunao wokovu wa milele ,wokovu ulio tayari kufuniliwa wakati wa mwisho.
  • Wokovu ni aina tatu:
  1. Wokovu uliopita (Past Salvation) Matendo 16:31, Warumi 10:9)
  • Tuliokolewa wakati tulipo mpokea Yesu Kristo
  1. Wokovu wa sasa (Present Salvation).
  • Tunaendelea kuokolewa kila saa(I Yohana 1:9, Wafilipi 2:12)
  • Tunaendelea kuokolewa, kukombolewa na damu ya Kristo inaendelea kutusafisha kila saa.
  1. Wokovu unaokuja (Future Salvation).
  • Tunaokolewa kabisa, kukombolewa kutoka kwa dhambi na hukumu. Huu wokovu unaokuja ndio uridhi wa milele. (Warumi 13:11,           Waebrania 1:14).

II.  KIINI CHA URIDHI WETU. (1 PETRO 1:3)

  1. Kiini cha uridhi wetu ni Mungu Baba, Baba wa Mwokozi wetu YESU KRISTO.
  • Mungu Baba ametuchangua kuokolewa na kupokea wokovu wa milele,yaani uridhi wa milele.
  1. Sababu ya Mwito wetu(1 Petro 1:3).
  • Rehema ya Mungu imetuchagua .(Tito 3:5).
  • Rehema ni nini? (Waefeso 2:4-5). Tulikuwa katika shida, maskini (Marko 10-Bartimayo).
  • Rehema ya Mungu ni nyingi zaidi (Kutoka 34:6, Zaburi 108:4, Mika 7:18, Maombolezo 3:22, Warumi 9:15, II Wakorintho 1:3)

III. JE, TUNATEKELEZA URITHI HUU WA MILELE AJE?

  • Mungu alitufanya kuzaliwa mara ya pili
  • Hili tubandilishwe, Mungu alituzaa upya katika Kristo (Yeremia 13:23, Zaburi 51:5, II Wakorintho 5:17, Waefeso 2:3, I Thess 1:10)
  • Unapomjua Kristo na kuweka Imani yako ndani yake, kunamabandiliko, kuzaliwa upya (I Petro 1:23, Yohana 3:3, 14-15, Hesabu 21)
  • Matokeo ya kuokoka, kuzaliwa upya ni “tumaini lililo hai” (I Petro 1:3)
  • Tumaini la dunia hii ni tumaini linalokufa (I Wakorintho 15:19)
  • Mauti inakata matumaini yote, lakini tumaini letu liko hai yaani Kristo Yesu. (2 Petro 3:13)

IV.  JE, KITU GANI KIMETUPATIA TUMAINI LA MILELE? (I PETRO 1:3)

  • Tumepokea urithi wa milele kwa njia ya kuzaliwa upya.
  • Kwa kuzaliwa mara ya pili tumepata tumaini ya milele. Tumaini letu limejengwa juu ya kufufuka kwa Kristo kutoka kwa wafu!! (Yohana 14:19)
  • Hivyo tunao urithi wa milele, kutoka kwa Mungu Baba, kwa sababu ya rehema yake, kupitia kuzaliwa mara ya pili.

MWISHO

  • Hata chochote kifanyike, majaribu yaje, tunao tumaini ya milele, tunao urithi wa milele mbinguni.
  • Je, umeokoka? Furahi katika majaribu na mangumu unayopitia, tunayo tumaini la milele. Hivyo tumsifu Mungu siku zote.
The following two tabs change content below.
Rev, Dr. Willy Mutiso is the Senior Pastor at First Baptist Athiriver. He is widely known for his practical and dynamic teaching style which helps people apply the timeless truths of Scripture to their everyday lives.

Latest posts by Rev, DR. Willy Mutiso (see all)

Rev, DR. Willy Mutiso

Rev, Dr. Willy Mutiso is the Senior Pastor at First Baptist Athiriver. He is widely known for his practical and dynamic teaching style which helps people apply the timeless truths of Scripture to their everyday lives.

Share
Published by
Rev, DR. Willy Mutiso

Recent Posts

DAMU YA UTAKASO.

MFULULIZO: AGANO LA UTAKASO. SOMO: KUTOKA 12:12-13.   Damu ya Yesu Kristo ndiyo mhuri wa…

2 days ago

KEY TO DIVINE SPEED.

SERIES: SUPERNATURAL ADVANCEMENT. TEXT: HABAKKUK 3:19.   The journey of fulfilling your destiny does not…

2 days ago

BE YE THANKFUL TO GOD.

SERIES: THROUGH THE BOOK OF COLOSSIANS. TEXT: COLOSSIANS 3:15   Thankfulness is a great attitude…

2 days ago

LEVELS OF THE ANOINTING.

SERIES: THE ANOINTING. TEXT: EZEKIEL 47:1-5   There are levels of the anointing and each…

6 days ago

UMETAKASWA KUPOKEA KIBALI.

MFULULIZO: AGANO LA UTAKASO. SOMO: ESTA 2:15-18.   Kibali cha Mungu ndicho kinacho watenga watoto…

1 week ago

THE GOD WHO SHIFTS THE HEAVENS IN YOUR FAVOR.

SERIES: THE GOD WHO NEVER FAILS. TEXT: HAGGAI 2:6-9.   God has the power to…

1 week ago