MFULULIZO: TUMAINI HAI.
SOMO: 1 Petro 2:9-12.
Mtume Petro anawaeleza waumini kwamba sisi NI WASAFIRI NA WAGENI duniani. Mgeni maana ni mtu anayeishi kwa muda katika nchi isiyo yake. Huyu mgeni ameishi katika nchi ya kigeni kwa muda kiasi amehitaji kuwa na nyumba ya kuishi na kufanya kazi lakini katika nchi ya ugeni. Lakini yeye si mwananchi.
Huyu mgeni hana haki ya kisheria na uwananchi.
Msafiri naye mpita njia, Yuko safarini kwenda kwingine.
Maneno haya mawili ndiyo mtume Petro anayatumia kueleza watoto wa Mungu walivyo hapa duniani.
Kwa kweli Dunia hii si kwetu, kwetu ni mbinguni-(Wafilipi 3:20)
“Kwa maana sisi wenyeji wetu uko mbinguni, kutoka huko tena tunatazamia Mwokozi Bwana Yesu Kristo.”
Tuko hapa duniani kiasi kuhitaji nyumba ya kukaa na kazi ya kutupatia riziki, Lakini makao yetu ya kudumu Yako mbinguni kwa Baba.
Sisi ni wageni, tunaishi katikati ya tamaduni za kigeni.
Sisi tunapita njia tukienda kwetu mbinguni.
Tabia yetu si ya ulimwengu huu, sisi tu watoto wa NURU ya Mungu.
Tunapoishi hapa duniani, tunaishi kama Wana wa mbinguni, tumezaliwa kimbinguni- (Wakolosai 3:1-3).
Kwa maana sisi ni wageni hapa duniani, kwa maana sisi ni wasafiri tabia zetu ni za mbinguni, si za Dunia hii.
Katika vifungu hivi Mtume Petro anatukumbusha mambo kadha. Hebu tutazame vikumbusho kwa wasafiri na wageni:-
UKUMBUSHO WA HALI YETU YA PALE KALE.
Maisha yetu ya kale yalikuwa Giza- (V. 9).
Maisha yetu ya kale yalikuwa aibu (V. 10).
Tulikuwa wafu mbele zake-(V. 10).
UKUMBUSHO WA HALI YETU YA SASA-(V. 10)
Sasa sisi ni viumbe wapya-(V. 9).
Sasa sisi ni ushirika mpya- sisi ni makuhani wa kifalme (royal priesthood)
Tumepewa tabia mpya.
Tumewekwa kiwango kingine.
UKUMBUSHO WA JINSI TULIVYO KATIKA UTUMISHI
V. 9-Tunahitaji kutangaza ukweli wa mwokozi wetu Yesu Kristo.
MWISHO.
MFULULIZO: MAISHA BILA VIZUIZI. SOMO: ZABURI 46:1. Biblia inatuakikishia kwamba Mungu wetu ni “Msaada…
SERIES: THE GOD WHO NEVER FAILS. TEXT: PROVERBS 3:5-6. Every destiny is a divine…
SERIES: THROUGH THE BOOK OF COLOSSIANS. TEXT: Colossians 3:5-10 We have put off the…
SERIES: THE GOD WE SERVE TEXT: 2nd SAMUEL 5:17-20 Breakthroughs are divine interventions that…
SERIES: DRAWING NEAR TO GOD TEXT: LAMENTATIONS 3:37 It reminds believers that God's word alone…
MFULULIZO: MAISHA BILA VIZUIZI. SOMO: 1 YOHANA 5:4. Wakristo wengi wanaishi maisha ya kushindwa…