MHUBIRI 3:1-15, MITHALI 3:5-6
UTANGULIZI
Mungu amempa kila mtu kila mahali kipawa cha wakati. Sisi zote tunaishi katika wakati. Hebu tujifunze:-
I. ANAYOTUFUNDISHA MUNGU JUU YA WAKATI (Mhubiri 3:1-15)
- Mungu, Yehova amempa kila mtu kila mahali katika nyakati zake wakati.
- Mungu ametupa sisi jana, leo na pengine kesho, hivyo hesabu leo kuwa maana sana.
- Jana imepita, kesho ni ahadi, leo ndiyo siku jema.
- Mungu amefanya kila kitu kizuri kwa wakati wake (V.11)
- Hivyo ni wewe utachangua kufadhaika hau kutofadhaika.
- Faidika na kazi ya mikono yako (V.9) kazi yako ndiyo inaeleza zaidi maisha yako.
- Mungu anao mpago wa ajabu kwa kila maisha ya kila mtu (v.10)
- Mungu ametupa uwezo wa kutazama mbele ya maisha ya leo.
- Mungu ameiweka milele (Eternity)ndani ya mioyo yetu.
- Mungu anatarajia kila mtu afanye mema katika kazi yake (v.12)
- Furahi na kufanya mema maadamu unapoishi.
- Mungu ametupa uwezo wa kujua kama kazi yetu ni jema hau mbaya (V11)
- Mungu anapenda sisi kufurahia kazi zetu.
- Ni karama ya Mungu kila mtu apate “Kula na kunywa na kujiburudisha” (V.13)
- Wakati unatubandilisha sana, lakini Mungu habadiliki kamwe, wala mpango wake kwetu.
- “Kila kazi aifanyayo Mungu itadumu milele” (v.14)
- Hata siku ya kufa Mungu ameitenga (V.19)
- Lakini mtu wa Mungu hawezi kufa mpaka kazi ya Bwana dani yake kukamilika.
- Ni haraka kushuku mambo ya Mungu kwa sababu ya uovu, udhalimu na ufisadi duniani (v.16)
- Lakini pamoja na uovu na udhalimu kila mahali, Mungu yupo enzini.
- Mungu anaye mipango ya ajabu (Warumi 8:28)
- Mungu anaruhusu dhiki, mateso na machungu ili kutukuza.
- Mazuri na mambaya yanamtukuza Mungu.
II. WAKATI UNABANDILISHA KILA KITU
- Kanuni tatu za kukua.
- Kukua ni kubandilika.
- Kila mabandiliko huleta mazuri hau mambaya.
- Mabandiliko ndiyo bei ya kukua.
- Watu hawapendi mabandiliko kwa sababu.
- Kutoeleweka
- Kubandilika huleta kupoteza.
- Watu wanatosheka na njia za kale
- Mabandiliko yako kila mahali.
- Wakati wa kupanda na wakati wa kuvuna.
- Wakati wa ujana na wakati wa uzee.
- Miili yetu inapata nguvu, baadaye udhaifu.
- Mabandiliko ni mema maana yanaleta kukua.
- Ukristo unaleta mabandiliko zaidi
- Kipofu anapata kuona
- Mpotevu anapatikana,
- Mfu anapata kuishi
- Tunabandilishwa tuwe kama Kristo.
III. BASI TUTAISHI AJE?
- Fanya kila siku kuhesabika.
- Furahia kila siku.
- Mungu atafanya kila jambo bora katika wakati wake.
- Kila jambo lina sababu yake. Ugojwa, ajali, uchungu, dhoruba, vita na mauti.
- Goja kwa subira Mungu akufunulie sababu ya masiha yako.
- Amua kumtumaini Mungu katika kila jambo (Mithali 3:5-6)
- Fahamu mambo na ukweli ufuatao:-
- Mungu bado anakupenda
- Biblia bado ni kweli
- Mungu anayajibu maombi
- Roho mtakatifu bado anawatafuta wenye dhambi, Kanisa litadumu milele. Mungu atazidi kubariki maubiri ya neno lake, Roho mtakatifu hatakuacha kamwe, Mungu anajua shida zako
- Kungali nafasi msalabani kwa ajili yako. Yesu Kristo bado anaokoa
MWISHO
- Kama bado hujaokoka, okoka sasa.
- Yesu Kristo bado anatafuta na kuokoa wenye dhambi.
- Nyakati zetu ziko mikononi mwa Mungu.
- Leo ndiyo siku ya maana kwako, fanya bidii leo kuhesabika.
- Yesu Kristo ni yeye yule jana na leo na hata milele (Waebrania 13:8)
The following two tabs change content below.
Rev, Dr. Willy Mutiso is the Senior Pastor at First Baptist Athiriver. He is widely known for his practical and dynamic teaching style which helps people apply the timeless truths of Scripture to their everyday lives.
Latest posts by Rev, DR. Willy Mutiso (see all)
- DAMU YA UTAKASO. - October 26, 2025
- KEY TO DIVINE SPEED. - October 26, 2025
- LEVELS OF THE ANOINTING. - October 22, 2025
