DANIEL Swahili Service

UTABIRI WA MWISHO KUTOKA KWA MUNGU

DANIELI 12:1-13

UTANGULIZI

Leo twatamatisha mfululizo wa ujumbe katika kitabu cha Danieli. Tunatazama ukweli tano kutoka kwa Biblia, tunapoona utabiri wa mwisho kutoka kwa Mungu. Hebu tuone:-

I.  UKWELI WA MUNGU; KUNA KITABU CHA UZIMA (12:1)

  • Swali ni ; Je, jina langu lipo katika kile kitabu?
  • Maranyingi Biblia inatueleza kwamba kuna kitabu ambacho kimeandikwa majina ya watu.
  • Mungu anafanya kazi na watu binafsi.
  • Maisha yako na jina lako nila maana sana mbele zake.
  • Majina yetu yameandikwa katika orodha mbalimbali kama ushirika, vyama, shule, kanisani, chuoni etc.
  • Lakini orodha ya majina iliyo maana zaidi ni kitabu cha uzima (The book of life)
  • Biblia inasema Mungu anayo orodha ya wale wameokoka, waliochnaguliwa tangu mwanzo (Waefeso.1:4)
  • Jina lako kuwa katika kitabu cha uzima ni furaha tele (Luka 10:20)
  • Kukosa kuwa katika kitabu cha uzima ni balaa kubwa (Ufunuo 20:15)
  • Madhehebu mengi yanawapa watu usalama wa uongo kwamba wameokoka-ubatizo,, kifaimara, kutoa fungu– lakini kitabu cha maana ni kitabu cha uzima (Mathayo 7:21-23)

II.  UKWELI WA MUNGU; KUTAKUWA NA KUYAMA HAINA MBILI (Danieli 12:2)

  • Swali ni ; Je, mimi nitakuwa katika kiyama cha wafu gani?
  • Ona jinsi Biblia inasema (Yohana 5:28-29, Ufunuo 20:6)
  • Miili hii tulio nayo inazeeka, kugonjeka, baadaye kufa.
  • Lakini mauti ya mwili sio mwisho wa kuishi.
  • Nafsi zetu zinaendelea kuishi, either binguni ama jihanamu.
  • Baadaye kutakuwa na ufufuo wa wafu haina mbili (Ufu.20)
  • Walio na Kristo watafufuliwa wapate uzima wa milele, wasio na Kristo watafufuliwa wapate aibu na kudharauliwa milele.
  • Jihanamu inaitwa mauti ya pili, mauti ya mwili ni mauti ya kwanza.
  • Hivyo kuna kuzaliwa haina mbili na mauti haina mbili (Yohana 3)

III. UKWELI WA MUNGU; NYOTA ZA KWELI NI WALE  WAWALETAO WENGI KWA KRISTO (Danieli 12:3)

  • Swali ni, Je, unawaleta wengine kwa Kristo?
  • Leo hii– wanaoitwa nyota (stars) ni movie stars, rock stars, sports stars, business stars, beauty stars, Annual academy awards– wanao tazama wale ma-stars wanaitwa stargazers.
  • Lakini “Nyota za Mungu” ni wale wanaowaongoza watu kwa Kristo (Wafilipi 2:15-16)
  • “Nyota” ungara katika giza, nyota zinang’ara kwa uaminifu, nyota zinaonyesha njia na muelekeo

 

IV. UKWELI WA MUNGU; MAARIFA YATAONGEZEKA WAKATI WA MWISHO (Danieli 12:4)

  • Swali ni ; Je, ninatazama ishara hizi?
  • Usafiri utaongezeka na maarifa, watu watasafiri inchi mpaka inchi nyingine (Today 1,800mph/300kph)

V.  UKWELI WA MUNGU: KUNA STAREHE NA DHAWABU KWA WATU WA MUNGU (Danieli 12:13)

  • Swali; Je, mimi nina uhusiano wa kibinafsi na Mungu?
  • Hatujui Danieli alikufa lini, lakini ni baada ya ufunuo huu wa mwisho.
  • Danieli aliishi siku zake za mwisho katika dhamana na hakikisho kwamba Mungu alimahidi starehe na dhawabu kubwa.
  • Je, wewe utaishi katika hakika kwamba ukifa utaishi milele na Kristo mbinguni.
  • Je, wewe uko na hakika umeokoka– maombi yako yako vipi? (Ufunuo 13:14)

 

MWISHO

  • Je, Jina lako liko katika kitabu cha uzima?
  • Je, una hakika juu ya wakovu wako?

 

The following two tabs change content below.
Rev, Dr. Willy Mutiso is the Senior Pastor at First Baptist Athiriver. He is widely known for his practical and dynamic teaching style which helps people apply the timeless truths of Scripture to their everyday lives.

Latest posts by Rev, DR. Willy Mutiso (see all)

2 thoughts on “UTABIRI WA MWISHO KUTOKA KWA MUNGU”

Leave a Reply to Pastor John M Balijura Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *